26. Tafsiri ya Hadiyth ya mwanamke mwenye mashavu ya kupauka

4- Hadiyth ya Jaabir (Radhiya Allaahu ´anh) haikutaja ni wakati gani jambo hili lilitokea. Aidha mwanamke huyu alikuwa ni mzee sana asiyetaraji tena kuolewa (na hivyo anaruhusiwa kuonesha uso tofauti na wengine) au ilitokea kabla ya kuteremshwa Aayah yenye kuwajibisha kujifunika. Aayah hiyo iko katika Suurat-ul-Ahzaab ambayo imeteremshwa miaka tano au siba baada ya Hijrah na swalah ya Idi iliwekwa katika Shari´ah miaka miwili baada ya Hijrah.

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Hijaab, uk. 33-34
  • Imechapishwa: 26/03/2017