Miongoni mwa wanawake wa Kiislamu wako ambao wanafanya unafiki katika Hijaab. Wanapokuwa katika jamii inayovaa Hijaab nao wanavaa Hijaab. Na wanapokuwa katika jamii isiyovaa Hijaab nao hawavai Hijaab. Miongoni mwao wako ambao wanavaa Hijaab wanapokuwa sehemu ya ummah na wanapoingia sehemu ya biashara, hospitali, anamzungumzisha mmoja katika masonara au mmoja wapo katika mafundi wa nguo za wanawake, basi anafunua uso wake na mikono yake kana kwamba yuko mbele ya mume wake au mmoja katika Mahram zake. Mcheni Allaah enyi mnaofanya mambo hayo.
Tumewashuhudia baadhi ya wanawake wanaofika kwenye uwanja wa ndege wanaotoka nje ya nchi ambao hawavai Hijaab isipokuwa pale ambapo ndege inadema katika moja ya viwanja vya ndege vya nchi hii. Ni kama kwamba Hijaab imekuwa ni katika desturi na sio katika mambo yaliyowekewa Shari´ah na dini hii.
Ee dada wa Kiislamu! Hakika Hijaab inakulinda na inakuhifadhi kutokamana na macho yenye sumu yanayotoka kwa wale ambao mioyoni mwao mna maradhi na mijibwawatu na isitoshe inakata zile tamaa zao. Hivyo basi, lazimiana nayo na shikamana nayo barabara. Usijali propaganda zenye kubabaisha zinazoipiga vita Hijaab na kuidogesha. Kwani hakika si vyengine wanakutakia shari. Allaah (Ta´ala) amesema:
وَيُرِيدُ الَّذِينَ يَتَّبِعُونَ الشَّهَوَاتِ أَن تَمِيلُوا مَيْلًا عَظِيمًا
“Wale wanaofuata matamanio wanataka mkengeuke, mkengeuko mkubwa mno.”[1]
[1] 04:27
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Tanbiyhaat, uk. 52
- Imechapishwa: 31/10/2019
Miongoni mwa wanawake wa Kiislamu wako ambao wanafanya unafiki katika Hijaab. Wanapokuwa katika jamii inayovaa Hijaab nao wanavaa Hijaab. Na wanapokuwa katika jamii isiyovaa Hijaab nao hawavai Hijaab. Miongoni mwao wako ambao wanavaa Hijaab wanapokuwa sehemu ya ummah na wanapoingia sehemu ya biashara, hospitali, anamzungumzisha mmoja katika masonara au mmoja wapo katika mafundi wa nguo za wanawake, basi anafunua uso wake na mikono yake kana kwamba yuko mbele ya mume wake au mmoja katika Mahram zake. Mcheni Allaah enyi mnaofanya mambo hayo.
Tumewashuhudia baadhi ya wanawake wanaofika kwenye uwanja wa ndege wanaotoka nje ya nchi ambao hawavai Hijaab isipokuwa pale ambapo ndege inadema katika moja ya viwanja vya ndege vya nchi hii. Ni kama kwamba Hijaab imekuwa ni katika desturi na sio katika mambo yaliyowekewa Shari´ah na dini hii.
Ee dada wa Kiislamu! Hakika Hijaab inakulinda na inakuhifadhi kutokamana na macho yenye sumu yanayotoka kwa wale ambao mioyoni mwao mna maradhi na mijibwawatu na isitoshe inakata zile tamaa zao. Hivyo basi, lazimiana nayo na shikamana nayo barabara. Usijali propaganda zenye kubabaisha zinazoipiga vita Hijaab na kuidogesha. Kwani hakika si vyengine wanakutakia shari. Allaah (Ta´ala) amesema:
وَيُرِيدُ الَّذِينَ يَتَّبِعُونَ الشَّهَوَاتِ أَن تَمِيلُوا مَيْلًا عَظِيمًا
“Wale wanaofuata matamanio wanataka mkengeuke, mkengeuko mkubwa mno.”[1]
[1] 04:27
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Tanbiyhaat, uk. 52
Imechapishwa: 31/10/2019
https://firqatunnajia.com/26-hijaab-za-kinafiki/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)