24- Abul-Qaasim Yahyaa bin As´ad bin Buush ametuhadithia: Abul-´Izz Ahmad bin ´Ubaydillaah bin Kaadis ametuhadithia: Abu ´Aliy Muhammad bin al-Husayn al-Jaaziriy ametuhadithia: Abul-Faraj al-Mu´aafaa bin Zakariyyaa al-Jariyriy ametuhadithia: Muhammad bin al-Qaasim al-Anbaariy ametuhadithia: Muhammad bin al-Marzabaan ametuhadithia: Abu ´Abdir-Rahmaan al-Jawhariy ametuhadithia: ´Ubaydullaah bin adh-Dhwahhaak ametuhadithia: al-Haytham bin ´Adiy ametuhadithia, kutoka kwa ´Awaanah bin al-Hakam aliyesema:
“Wakati ´Umar bin ´Abdil-´Aziyz alipokuwa khalifah kundi la wanashairi walikuja kwake. Wakasimama nje ya mlango wake kwa masiku kadhaa pasi na kupewa idhini. Siku moja wakati walipokuwa katika hali hiyo na wameazimia kurudi. Ndipo ´Adiy bin Artwa’ah akapita karibu yao ambapo Jariyr akamwambia:
Ee mpandaji unayeendesha kipando chako
huu ni wakati wako – mimi wakati wangu umeshapita
Msalimie khalifa wetu ukikutana naye
kwamba nimekuwa kama mfungwa karibu na mlango
Usizisahau haja zetu – naomba usamehewe
nimekuwa mbali na familia yangu na nchi yangu kwa muda mrefu
´Adiy akaenda kwa ´Umar na kusema: “Ee kiongozi wa waumini! Wanashairi wako nje ya mlango wako. Mishale yao ina sumu na maneno yao ni yenye kukubalika.” Akasema: “Ole wako, ee ´Adiy! Mimi ninahusiana nini na wanashairi?” Akasema: “Allaah amtie nguvu kiongozi wa waumini! Wakati Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliposifiwa alitoa. Hakika una kiigizo chema kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).” Akasema: “Vipi yaani?” ´Adiy akasema: “al-´Abbaas bin Mirdaas as-Sulamiy alimsifu ambapo akampa koti. “ ´Umar akauliza: “Unaweza kuelezea chochote katika yale aliyosema?” Akajibu: “Ndio:
Nimekuona, ee kiumbe bora kabisa
eneza na funza Kitabu kilichokuja kwa haki
Umetuwekea katika Shari´ah dini ya mwongozo
baada ya kuwa wapotofu na wenye giza kunako haki
Umekiangazia kitu kilicho na ukungu kwa dalili
na umezima moto uwakao
Ni nani awezaye kunifikishia salamu kwa Mtume Muhammad
kila mmoja atalipwa kwa kile alichotanguliza
Umeinyoosha njia ya haki baada ya kupinda kwake
Nguzo yake ilikuwa imebomoka tokea hapo kitambo
Ametakasika Mola wetu aliye juu ya ´Arshi
Nafasi ya Allaah iko juu na ni kubwa[1]
Kisha akataja yaliyobaki.
[1] Ibn ´Abdi Rabbih al-Andalusiy katika ”al-´Aqd al-Fariyd” (1/205). adh-Dhahabiy amesema:
”al-Haytham bin ´Adiy ni dhaifu.” (al-´Uluww, uk. 42)
- Mhusika: Imaam Muwaffaq-ud-Diyn bin Qudaamah al-Maqdisiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ithbaatu Swifat-il-´Uluww, uk. 106-108
- Imechapishwa: 07/06/2018
24- Abul-Qaasim Yahyaa bin As´ad bin Buush ametuhadithia: Abul-´Izz Ahmad bin ´Ubaydillaah bin Kaadis ametuhadithia: Abu ´Aliy Muhammad bin al-Husayn al-Jaaziriy ametuhadithia: Abul-Faraj al-Mu´aafaa bin Zakariyyaa al-Jariyriy ametuhadithia: Muhammad bin al-Qaasim al-Anbaariy ametuhadithia: Muhammad bin al-Marzabaan ametuhadithia: Abu ´Abdir-Rahmaan al-Jawhariy ametuhadithia: ´Ubaydullaah bin adh-Dhwahhaak ametuhadithia: al-Haytham bin ´Adiy ametuhadithia, kutoka kwa ´Awaanah bin al-Hakam aliyesema:
“Wakati ´Umar bin ´Abdil-´Aziyz alipokuwa khalifah kundi la wanashairi walikuja kwake. Wakasimama nje ya mlango wake kwa masiku kadhaa pasi na kupewa idhini. Siku moja wakati walipokuwa katika hali hiyo na wameazimia kurudi. Ndipo ´Adiy bin Artwa’ah akapita karibu yao ambapo Jariyr akamwambia:
Ee mpandaji unayeendesha kipando chako
huu ni wakati wako – mimi wakati wangu umeshapita
Msalimie khalifa wetu ukikutana naye
kwamba nimekuwa kama mfungwa karibu na mlango
Usizisahau haja zetu – naomba usamehewe
nimekuwa mbali na familia yangu na nchi yangu kwa muda mrefu
´Adiy akaenda kwa ´Umar na kusema: “Ee kiongozi wa waumini! Wanashairi wako nje ya mlango wako. Mishale yao ina sumu na maneno yao ni yenye kukubalika.” Akasema: “Ole wako, ee ´Adiy! Mimi ninahusiana nini na wanashairi?” Akasema: “Allaah amtie nguvu kiongozi wa waumini! Wakati Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliposifiwa alitoa. Hakika una kiigizo chema kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).” Akasema: “Vipi yaani?” ´Adiy akasema: “al-´Abbaas bin Mirdaas as-Sulamiy alimsifu ambapo akampa koti. “ ´Umar akauliza: “Unaweza kuelezea chochote katika yale aliyosema?” Akajibu: “Ndio:
Nimekuona, ee kiumbe bora kabisa
eneza na funza Kitabu kilichokuja kwa haki
Umetuwekea katika Shari´ah dini ya mwongozo
baada ya kuwa wapotofu na wenye giza kunako haki
Umekiangazia kitu kilicho na ukungu kwa dalili
na umezima moto uwakao
Ni nani awezaye kunifikishia salamu kwa Mtume Muhammad
kila mmoja atalipwa kwa kile alichotanguliza
Umeinyoosha njia ya haki baada ya kupinda kwake
Nguzo yake ilikuwa imebomoka tokea hapo kitambo
Ametakasika Mola wetu aliye juu ya ´Arshi
Nafasi ya Allaah iko juu na ni kubwa[1]
Kisha akataja yaliyobaki.
[1] Ibn ´Abdi Rabbih al-Andalusiy katika ”al-´Aqd al-Fariyd” (1/205). adh-Dhahabiy amesema:
”al-Haytham bin ´Adiy ni dhaifu.” (al-´Uluww, uk. 42)
Mhusika: Imaam Muwaffaq-ud-Diyn bin Qudaamah al-Maqdisiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Ithbaatu Swifat-il-´Uluww, uk. 106-108
Imechapishwa: 07/06/2018
https://firqatunnajia.com/26-dalili-ya-ishirini-na-nne-kutoka-katika-sunnah-kwamba-allaah-yuko-juu-ya-viumbe/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)