1- Kujizuia kusafiri katika mwezi wa Swafar na kuacha kuanza matendo ndani yake, kama vile kuoa, jimaa na mengineyo.
2- Kuacha kusafiri pindi mwezi unapofifia na pindi mwezi unapokuwa katika alama ya nge.
3- Kuacha kusafisha nyumba wakati mtu anapokuwa katika hali ya kusafiri.
4- Mtu anaswali Rak´ah mbili wakati anapotoka kwenda katika hajj ambapo anasoma katika Rak´ah ya kwanza “al-Kaafiruun” baada ya kusoma al-Faatihah na katika Rak´ah ya pili anasoma “al-Ikhlaasw”. Anapomaliza kufanya hivo anasema:
اللهم بك انتشرت وإليك توجهت
“Ee Allaah! Hakika mimi nimetoka kwa ajili Yako na Kwako ndiko nimeelekea… “
Baada ya hapo anasoma Aayat-ul-Kursiy, Suurah al-Ikhlaasw, al-Falaq na an-Naas na nyenginezo zilizotajwa katika baadhi ya vitabu vya Fiqh.
5- Mtu kuswali Rak´ah nne.
6- Yule anayetaka kufanya hajj pindi anapotoka nyumbani kwake anasoma mwisho wa Suurah “Aal ´Imraan”, “Aayat-ul-Kursiy”, “al-Qadr” na “al-Faatihah”. Wanadai kwamba kufanya hivo kunatatua haja za duniani na Aakhirah.
7- Kumtaja Allaah na kusema “Allaahu Akbar” kwa sauti ya juu wakati mahujaji wanapoanza safari zao na pindi wanaporudi.
8- Adhaana wakati wa kuwaaga.
9- Kumfanya ngamia kutokea Misri na Syria akiwa na pazia ya Ka´bah na kusherehekea kwa kuizunguka[1].
10- Baadhi ya miji inawaaga mahujaji kwa muziki.
11- Mtu kusafiri peke yake kwa madai kwamba anaanasika kwa Allaah, kama wanavodai baadhi ya Suufiyyah.
12- Kusafiri bila ya kuchukua masurufu kwa kurekebisha madai ya kutawakali.
13- Kusafiri kwa ajili ya kutembelea makaburi ya Mitume na waja wema.
14- Mwanamume kumuoa mwanamke ambaye tayari ameshaolewa akitaka kuhiji na akawa hana Mahram. Hivyo anamuoa ili yeye ndiye awe kama Mahram wake[2].
15- Kufanya uhusiano wa kidugu baina ya mwanamke na mwanaume ambaye ni ajinabi kwake ili – kama wanavodai – awe Mahram wake. Kisha mwanaume huyo anatangamana naye mwanamke huyo kama anavyotangamana na Mahaarim zake.
16- Mwanamke kusafiri pamoja na kundi la wanawake wenzake waaminifu – kama wanavodai – pasi na kuwa na Mahram. Kwa mfano utamkuta mmoja ndiye yuko na Mahram ambapo wanadai kuwa mwanaume huyo ndiye Mahram wa wote hao.
17- Kuchukua kodi kutoka kwa mahujaji ambao wamekusudia kutekeleza faradhi ya hajj.
18- Msafiri kuswali Rak´ah mbili kila mahali anapotua. Kisha anasema:
رَّبِّ أَنزِلْنِي مُنزَلًا مُّبَارَكًا وَأَنتَ خَيْرُ الْمُنزِلِينَ
“Ee Mola wangu! Niteremshe mteremko wenye baraka! Nawe ni Mbora wa wenye kuteremsha.”[3]
19- Msafiri kusoma Suurah “al-Ikhlaasw” mara kumi na moja kila mahali anapotua, “Aayat-ul-Kursiy” mara moja na Aayah “Hawakumuadhimisha Allaah ukweli wa kumuadhimisha![4]” mara moja.
20- Msafiri kula kitunguu saumu kila mahali atapotua.
21- Kusafiri kwenda maeneo fulani kwa ajili ya kukusudia kheri ya sehemu hiyo. Hilo halikupendekezwa na Shari´ah. Kwa mfano sehemu ambazo inasemekana kuna athari za Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Kama inavosemwa juu ya mwamba wa Yerusalemu, msikiti wa mguu kabla ya Dameski na makaburi ya Mitume na waja wema[5].
22- Kuzielekeza silaha wakati mtu anapofika Tabuuk.
[1] Bid´ah hii imetokomea kwa miaka mingi na himdi zote anastahiki Allaah. Hata hivyo kumekuja badala yake Bid´ah nyenginezo. Katika al-Baajuriy imekuja kwamba Ibn-ul-Qaasim amesema:
“Ni haramu kukatakata vipande ile pazia inayotambulika na pazia ya sehemu ya kusimama Ibraahiym.” (1/41)
[2] Hii na inayofuata ni miongoni mwa Bid´ah mbaya kabisa kutokana na ule udanganyifu juu ya Shari´ah na kujiweka katika kutumbukia katika madhambi mabaya.
[3] 23:29
[4] 39:66
[5] Imesihi kutoka kwa ´Umar bin al-Khattwaab (Radhiya Allaahu ´anh) kwamba aliwaona watu wakati wa hajj yake wanakimbilia sehemu fulani. Akasema: “Ni kitu gan?” Kukasemwa: “Ni msikiti ambao aliswali ndani yake Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).” Ndipo akasema: “Hivi ndivo walivyoangamia watu wa Kitabu pindi walipozifanya athari za Mitume wao kuwa ni masinagogi na makanisa. Yule ambaye itamtokea muda wa swalah ukamkuta huko basi na aswali. Vinginevyo asiswali.”
- Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Manaasik-ul-Hajj wal-´Umrah, uk. 45-47
- Imechapishwa: 21/07/2018
1- Kujizuia kusafiri katika mwezi wa Swafar na kuacha kuanza matendo ndani yake, kama vile kuoa, jimaa na mengineyo.
2- Kuacha kusafiri pindi mwezi unapofifia na pindi mwezi unapokuwa katika alama ya nge.
3- Kuacha kusafisha nyumba wakati mtu anapokuwa katika hali ya kusafiri.
4- Mtu anaswali Rak´ah mbili wakati anapotoka kwenda katika hajj ambapo anasoma katika Rak´ah ya kwanza “al-Kaafiruun” baada ya kusoma al-Faatihah na katika Rak´ah ya pili anasoma “al-Ikhlaasw”. Anapomaliza kufanya hivo anasema:
اللهم بك انتشرت وإليك توجهت
“Ee Allaah! Hakika mimi nimetoka kwa ajili Yako na Kwako ndiko nimeelekea… ”
Baada ya hapo anasoma Aayat-ul-Kursiy, Suurah al-Ikhlaasw, al-Falaq na an-Naas na nyenginezo zilizotajwa katika baadhi ya vitabu vya Fiqh.
5- Mtu kuswali Rak´ah nne.
6- Yule anayetaka kufanya hajj pindi anapotoka nyumbani kwake anasoma mwisho wa Suurah “Aal ´Imraan”, “Aayat-ul-Kursiy”, “al-Qadr” na “al-Faatihah”. Wanadai kwamba kufanya hivo kunatatua haja za duniani na Aakhirah.
7- Kumtaja Allaah na kusema “Allaahu Akbar” kwa sauti ya juu wakati mahujaji wanapoanza safari zao na pindi wanaporudi.
8- Adhaana wakati wa kuwaaga.
9- Kumfanya ngamia kutokea Misri na Syria akiwa na pazia ya Ka´bah na kusherehekea kwa kuizunguka[1].
10- Baadhi ya miji inawaaga mahujaji kwa muziki.
11- Mtu kusafiri peke yake kwa madai kwamba anaanasika kwa Allaah, kama wanavodai baadhi ya Suufiyyah.
12- Kusafiri bila ya kuchukua masurufu kwa kurekebisha madai ya kutawakali.
13- Kusafiri kwa ajili ya kutembelea makaburi ya Mitume na waja wema.
14- Mwanamume kumuoa mwanamke ambaye tayari ameshaolewa akitaka kuhiji na akawa hana Mahram. Hivyo anamuoa ili yeye ndiye awe kama Mahram wake[2].
15- Kufanya uhusiano wa kidugu baina ya mwanamke na mwanaume ambaye ni ajinabi kwake ili – kama wanavodai – awe Mahram wake. Kisha mwanaume huyo anatangamana naye mwanamke huyo kama anavyotangamana na Mahaarim zake.
16- Mwanamke kusafiri pamoja na kundi la wanawake wenzake waaminifu – kama wanavodai – pasi na kuwa na Mahram. Kwa mfano utamkuta mmoja ndiye yuko na Mahram ambapo wanadai kuwa mwanaume huyo ndiye Mahram wa wote hao.
17- Kuchukua kodi kutoka kwa mahujaji ambao wamekusudia kutekeleza faradhi ya hajj.
18- Msafiri kuswali Rak´ah mbili kila mahali anapotua. Kisha anasema:
رَّبِّ أَنزِلْنِي مُنزَلًا مُّبَارَكًا وَأَنتَ خَيْرُ الْمُنزِلِينَ
“Ee Mola wangu! Niteremshe mteremko wenye baraka! Nawe ni Mbora wa wenye kuteremsha.”[3]
19- Msafiri kusoma Suurah “al-Ikhlaasw” mara kumi na moja kila mahali anapotua, “Aayat-ul-Kursiy” mara moja na Aayah “Hawakumuadhimisha Allaah ukweli wa kumuadhimisha![4]” mara moja.
20- Msafiri kula kitunguu saumu kila mahali atapotua.
21- Kusafiri kwenda maeneo fulani kwa ajili ya kukusudia kheri ya sehemu hiyo. Hilo halikupendekezwa na Shari´ah. Kwa mfano sehemu ambazo inasemekana kuna athari za Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Kama inavosemwa juu ya mwamba wa Yerusalemu, msikiti wa mguu kabla ya Dameski na makaburi ya Mitume na waja wema[5].
22- Kuzielekeza silaha wakati mtu anapofika Tabuuk.
[1] Bid´ah hii imetokomea kwa miaka mingi na himdi zote anastahiki Allaah. Hata hivyo kumekuja badala yake Bid´ah nyenginezo. Katika al-Baajuriy imekuja kwamba Ibn-ul-Qaasim amesema:
“Ni haramu kukatakata vipande ile pazia inayotambulika na pazia ya sehemu ya kusimama Ibraahiym.” (1/41)
[2] Hii na inayofuata ni miongoni mwa Bid´ah mbaya kabisa kutokana na ule udanganyifu juu ya Shari´ah na kujiweka katika kutumbukia katika madhambi mabaya.
[3] 23:29
[4] 39:66
[5] Imesihi kutoka kwa ´Umar bin al-Khattwaab (Radhiya Allaahu ´anh) kwamba aliwaona watu wakati wa hajj yake wanakimbilia sehemu fulani. Akasema: “Ni kitu gan?” Kukasemwa: “Ni msikiti ambao aliswali ndani yake Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).” Ndipo akasema: “Hivi ndivo walivyoangamia watu wa Kitabu pindi walipozifanya athari za Mitume wao kuwa ni masinagogi na makanisa. Yule ambaye itamtokea muda wa swalah ukamkuta huko basi na aswali. Vinginevyo asiswali.”
Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Manaasik-ul-Hajj wal-´Umrah, uk. 45-47
Imechapishwa: 21/07/2018
https://firqatunnajia.com/24-bidah-kabla-ya-ihraam/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)