Shari´ah imeharamisha kumpa mtoto majina yafuatayo:
1- Waislamu wameafikiana[1] juu ya uharamu wa majina yote yanayoashiria kuwa mtu ni mja wa mwingine badala ya Allaah (Ta´ala). Haijalishi kitu ikiwa ni jua, mzimu, mtu au kitu kingine. Mfano wa majina hayo ya haramu ni kama ´Abdur-Rasuul, ´Abdun-Nabiy, ´Abdu ´Aliy, ´Abdul-Husayn, ´Abdul-Amiyr likiashiria kiongozi wa waumini ´Aliy bin Abiy Twaalib (Radhiya Allaahu ´anh) na ´Abdus-Swaahib likiashiria al-Mahdiy anayesubiriwa. Haya ni majina ya Raafidhwah.
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliyabadilisha majina yote yaliyo na uja wa asiyekuwa Allaah. Baadhi ya majina hayo ni ´Abdul-´Uzza, ´Abdul-Ka´bah, ´Abdu Shams na ´Abdul-Haarith.
Ndani ya sampuli hii kunaingia vilevile jina kama Ghulaam-ur-Rasuul na Ghulaam Muhammad linaloashiria “mja wa Mtume”.
Kwa mujibu wa maoni sahihi vilevile imekatazwa kuitwa ´Abdul-Muttwalib.
Katika makosa haya kunaingia vilevile majina yenye uja ambayo mtu anafikiria makosa kwamba ni majina ya Allaah (Ta´ala). Mfano wa majina hayo ni ´Abdul-Maqswuud, ´Abdus-Sattaar, ´Abdul-Mawjuud, ´Abdul-Huwa, ´Abdul-Mursil, ´Abdul-Waahid na ´Abdul-Twaalib. Majina haya yana makosa kwa mitazamo miwili:
Wa kwanza: Haijuzu kumwita Allaah (Ta´ala) kwa jina lisilokuwa na dalili katika Qur-aan na Sunnah.
Wa pili: Haijuzu kutoa jina linaloonyesha kuwa uja anafanyiwa Allaah ikiwa Allaah hakujiita nalo Mwenyewe wala Mtume Wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
[1] Tazama “Maraatib-ul-Ijmaa´”, uk. 154, ya Ibn Hamz na “Majmuu´-ul-Fataawaa” (01/378-379) ya Ibn Taymiyyah.
- Mhusika: ´Allaamah Bakr bin ´Abdillaah Abu Zayd
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Tasmiyat-ul-Mawluwd, uk. 21-22
- Imechapishwa: 18/03/2017
Shari´ah imeharamisha kumpa mtoto majina yafuatayo:
1- Waislamu wameafikiana[1] juu ya uharamu wa majina yote yanayoashiria kuwa mtu ni mja wa mwingine badala ya Allaah (Ta´ala). Haijalishi kitu ikiwa ni jua, mzimu, mtu au kitu kingine. Mfano wa majina hayo ya haramu ni kama ´Abdur-Rasuul, ´Abdun-Nabiy, ´Abdu ´Aliy, ´Abdul-Husayn, ´Abdul-Amiyr likiashiria kiongozi wa waumini ´Aliy bin Abiy Twaalib (Radhiya Allaahu ´anh) na ´Abdus-Swaahib likiashiria al-Mahdiy anayesubiriwa. Haya ni majina ya Raafidhwah.
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliyabadilisha majina yote yaliyo na uja wa asiyekuwa Allaah. Baadhi ya majina hayo ni ´Abdul-´Uzza, ´Abdul-Ka´bah, ´Abdu Shams na ´Abdul-Haarith.
Ndani ya sampuli hii kunaingia vilevile jina kama Ghulaam-ur-Rasuul na Ghulaam Muhammad linaloashiria “mja wa Mtume”.
Kwa mujibu wa maoni sahihi vilevile imekatazwa kuitwa ´Abdul-Muttwalib.
Katika makosa haya kunaingia vilevile majina yenye uja ambayo mtu anafikiria makosa kwamba ni majina ya Allaah (Ta´ala). Mfano wa majina hayo ni ´Abdul-Maqswuud, ´Abdus-Sattaar, ´Abdul-Mawjuud, ´Abdul-Huwa, ´Abdul-Mursil, ´Abdul-Waahid na ´Abdul-Twaalib. Majina haya yana makosa kwa mitazamo miwili:
Wa kwanza: Haijuzu kumwita Allaah (Ta´ala) kwa jina lisilokuwa na dalili katika Qur-aan na Sunnah.
Wa pili: Haijuzu kutoa jina linaloonyesha kuwa uja anafanyiwa Allaah ikiwa Allaah hakujiita nalo Mwenyewe wala Mtume Wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
[1] Tazama “Maraatib-ul-Ijmaa´”, uk. 154, ya Ibn Hamz na “Majmuu´-ul-Fataawaa” (01/378-379) ya Ibn Taymiyyah.
Mhusika: ´Allaamah Bakr bin ´Abdillaah Abu Zayd
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Tasmiyat-ul-Mawluwd, uk. 21-22
Imechapishwa: 18/03/2017
https://firqatunnajia.com/24-aina-ya-kwanza-ya-majina-ya-haramu/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)