Jina la Uislamu lilikuwa linatumika mwanzoni mwa Uislamu. Kipindi hicho kulikuwa hakutambuliki kujinasibisha katika kitu kingine mbali na Uislamu. Wakati kulipojitokeza Bid´ah, kukaenea matamanio na kila mzushi akajitenga mbali na Uislamu ndipo wema wetu waliotangulia wakalazimika kudhihirisha majina yao yaliyowekwa katika Shari´ah ambayo yanawapambanua na wapotevu wengineo. Kuanzia hapo wakaanza kujiita kwa majina yaliyopokelewa katika maandiko. Mfano wa majina hayo ni “al-Jamaa´ah” (mkusanyiko), al-Firqah an-Naajiyah” (kundi lililookoka) na at-Twaaifah al-Mansuurah” (kundi lililonusuriwa).
Vivyo hivyo wakajiita kwa yale waliyoshikamana nayo katika kutendea kazi Sunnah ambazo zimepewa mgongo na wengine. Mfano wa majina hayo ni Salaf, Ahl-ul-Hadiyth, Ahl-ul-Athar na Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah.
Wamejiita majina hayo kutokana na sababu nyingi. Shaykh Bakr bin ´Abdillaah Abu Zayd (Rahimahu Allaah) ametaja baadhi yake katika kitabu chake kitukufu: “Hukm-ul-Intimaa´ ilaal-Firaq wal-Ahzaab wal-Jama´aat-il-Islaamiyyah”. Miongoni mwazo:
1- Nisba hizi hazikutengana na Ummah wa Kiislamu tangu kuundwaa kwake kwa mujibu wa mfumo wa kinabii.
2- Nisba hizi zimekusanya Uislamu mzima.
3- Ni majina halisi.
4- Yamethibiti katika Sunnah Swahiyh.
5- Yako ambayo hayakutokea isipokuwa katika kuwakabili Ahl-ul-Ahwaa´ katika kurudisha Bid´ah na upotevu wao kwa ajili ya kujipambanua nao.
Utaona kuwa wakati ilipodhihiri Bid´ah basi Ah-ul-Haqq walipambanuka kwa Sunnah. Wakasema kuwa wao ni Ahl-us-Sunnah. Wakati rai iliposhika mkondo ndipo wakapambanuka kwa Hadiyth na Athar. Matokeo yake wakasema kuwa wao ni Ahl-ul-Hadiyth wal-Athar.
6- Majina haya hayawalinganii kufanya ushabiki kwa mtu mbali na Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
7- Majina haya hayapelekei katika Bid´ah, maasi, kufanya ushabiki kwa mtu wala kundi fulani.
8- Kujenga kwao mapenzi na chuki, urafiki na uadui ni kutokana na Uislamu na sio kitu kingine[1].
[1] ”Hukm-ul-Intimaa´ ilaal-Firaq”, uk. 31-33
- Mhusika: Shaykh ´Abdus-Salaam bin Barjas
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Usuwl-ud-Da´wah as-Salafiyyah, uk. 57-59
- Imechapishwa: 18/08/2020
Jina la Uislamu lilikuwa linatumika mwanzoni mwa Uislamu. Kipindi hicho kulikuwa hakutambuliki kujinasibisha katika kitu kingine mbali na Uislamu. Wakati kulipojitokeza Bid´ah, kukaenea matamanio na kila mzushi akajitenga mbali na Uislamu ndipo wema wetu waliotangulia wakalazimika kudhihirisha majina yao yaliyowekwa katika Shari´ah ambayo yanawapambanua na wapotevu wengineo. Kuanzia hapo wakaanza kujiita kwa majina yaliyopokelewa katika maandiko. Mfano wa majina hayo ni “al-Jamaa´ah” (mkusanyiko), al-Firqah an-Naajiyah” (kundi lililookoka) na at-Twaaifah al-Mansuurah” (kundi lililonusuriwa).
Vivyo hivyo wakajiita kwa yale waliyoshikamana nayo katika kutendea kazi Sunnah ambazo zimepewa mgongo na wengine. Mfano wa majina hayo ni Salaf, Ahl-ul-Hadiyth, Ahl-ul-Athar na Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah.
Wamejiita majina hayo kutokana na sababu nyingi. Shaykh Bakr bin ´Abdillaah Abu Zayd (Rahimahu Allaah) ametaja baadhi yake katika kitabu chake kitukufu: “Hukm-ul-Intimaa´ ilaal-Firaq wal-Ahzaab wal-Jama´aat-il-Islaamiyyah”. Miongoni mwazo:
1- Nisba hizi hazikutengana na Ummah wa Kiislamu tangu kuundwaa kwake kwa mujibu wa mfumo wa kinabii.
2- Nisba hizi zimekusanya Uislamu mzima.
3- Ni majina halisi.
4- Yamethibiti katika Sunnah Swahiyh.
5- Yako ambayo hayakutokea isipokuwa katika kuwakabili Ahl-ul-Ahwaa´ katika kurudisha Bid´ah na upotevu wao kwa ajili ya kujipambanua nao.
Utaona kuwa wakati ilipodhihiri Bid´ah basi Ah-ul-Haqq walipambanuka kwa Sunnah. Wakasema kuwa wao ni Ahl-us-Sunnah. Wakati rai iliposhika mkondo ndipo wakapambanuka kwa Hadiyth na Athar. Matokeo yake wakasema kuwa wao ni Ahl-ul-Hadiyth wal-Athar.
6- Majina haya hayawalinganii kufanya ushabiki kwa mtu mbali na Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
7- Majina haya hayapelekei katika Bid´ah, maasi, kufanya ushabiki kwa mtu wala kundi fulani.
8- Kujenga kwao mapenzi na chuki, urafiki na uadui ni kutokana na Uislamu na sio kitu kingine[1].
[1] ”Hukm-ul-Intimaa´ ilaal-Firaq”, uk. 31-33
Mhusika: Shaykh ´Abdus-Salaam bin Barjas
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Usuwl-ud-Da´wah as-Salafiyyah, uk. 57-59
Imechapishwa: 18/08/2020
https://firqatunnajia.com/23-ndipo-wakalazimika-kujiita-kwa-majina-haya/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)