23. Dalili ya kwamba Allaah ameumba Pepo kwa mkono Wake

23- Imaam ´Uthmaan bin Ibraahiym ametuhadithia kwa kutusomea: Ahmad bin Ibraahiym ametuhadithia: Ismaa´ily ametuhadithia: Abuu Yahyaa al-´Aaliy ametuhadithia: Ahmad bin ´Amr bin as-Sarj ametuhadithia: Ahmad bin Muhammad bin Manswuur bin al-Husayn bin ´Aliy ametuhadithia: Muhammad bin ´Aliy al-Haafidhw ametuhadithia Isfaraayiyn: ´Abdur-Rahmaan bin Ahmad bin Muhammad bin al-Hajjaaj bin Raashid bin Sa´d ametuhadithia Misri: Ahmad bin ´Amr bin as-Saraj ametuhadithia: Khaali wa Abuur-Rajaa´ ´Abdur-Rahmaan bin ´Abdil-Hamiyd al-Muhriy al-Miswriy ametuhadithia: Yahyaa bin Ayyuub ametuhadithia, kutoka kwa Daawuud bin Abiy Hind, kutoka kwa Anas bin Maalik (Radhiya Allaahu ´anh) aliyesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Allaah (´Azza wa Jall) ameumba Pepo kwa mkono Wake na ameipigia marufu kwa kila mshirikina na mwenye kunywa mlevi.”[1]

[1] Ibn Mandah katika ”ar-Radd ´alaal-Jahmiyyah”, uk. 77.

  • Mhusika: Imaam Abu Ismaa´iyl ´Abdullaah bin Muhammad al-Answaariy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Arba´uun fiy Dalaa-il-it-Tawhiyd, uk. 53
  • Imechapishwa: 29/01/2017