Allaah (´Azza wa Jall) amesema:
وَلَا تُبَاشِرُوهُنَّ وَأَنتُمْ عَاكِفُونَ فِي الْمَسَاجِدِ
“Na wala msichanganyike nao hali ya kuwa nyinyi ni wenye kukaa I’tikaaf misikitini.”[1]
Haya ni makatazo kutoka kwa Allaah (´Azza wa Jall). Mtu anayefanya I´tikaaf haijuzu kwake kufanya jimaa na wanawake na wala haijuzu hata kubusu. Mzee aliye na matamanio dhaifu inafaa kwake kubusu. Lakini mtu anayefanya I´tikaaf haifai kwake kubusu wala kukumbatia katika hali yoyote. Hayo ni haramu. Allaah (Ta´ala) amesema:
تِلْكَ حُدُودُ اللَّـهِ
“Hiyo ni mipaka ya Allaah.”[2]
Kitendo hichi ni katika mipaka ya Allaah. Yule mwenye kuchanganyika na mwanamke iliali ni mwenye kufanya I´tikaaf amevuka mpaka wa Allaah. Allaah (Ta´ala) amesema:
تِلْكَ حُدُودُ اللَّـهِ فَلَا تَقْرَبُوهَا
“Hiyo ni mipaka ya Allaah, hivyo basi msiikaribie.”[3]
Hii ni dalili inayofahamisha kuwa ni haramu kuchanganyika na wanawake wakati wa I´tikaaf na ni moja katika mipaka ya Allaah aliyoiharamisha.
[1] 02:187
[2] 02:187
[3] 02:187
- Mhusika: ´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Tafsiyr Aayaat-is-Swiyaam, uk. 40-41
- Imechapishwa: 02/06/2017
Allaah (´Azza wa Jall) amesema:
وَلَا تُبَاشِرُوهُنَّ وَأَنتُمْ عَاكِفُونَ فِي الْمَسَاجِدِ
“Na wala msichanganyike nao hali ya kuwa nyinyi ni wenye kukaa I’tikaaf misikitini.”[1]
Haya ni makatazo kutoka kwa Allaah (´Azza wa Jall). Mtu anayefanya I´tikaaf haijuzu kwake kufanya jimaa na wanawake na wala haijuzu hata kubusu. Mzee aliye na matamanio dhaifu inafaa kwake kubusu. Lakini mtu anayefanya I´tikaaf haifai kwake kubusu wala kukumbatia katika hali yoyote. Hayo ni haramu. Allaah (Ta´ala) amesema:
تِلْكَ حُدُودُ اللَّـهِ
“Hiyo ni mipaka ya Allaah.”[2]
Kitendo hichi ni katika mipaka ya Allaah. Yule mwenye kuchanganyika na mwanamke iliali ni mwenye kufanya I´tikaaf amevuka mpaka wa Allaah. Allaah (Ta´ala) amesema:
تِلْكَ حُدُودُ اللَّـهِ فَلَا تَقْرَبُوهَا
“Hiyo ni mipaka ya Allaah, hivyo basi msiikaribie.”[3]
Hii ni dalili inayofahamisha kuwa ni haramu kuchanganyika na wanawake wakati wa I´tikaaf na ni moja katika mipaka ya Allaah aliyoiharamisha.
[1] 02:187
[2] 02:187
[3] 02:187
Mhusika: ´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Tafsiyr Aayaat-is-Swiyaam, uk. 40-41
Imechapishwa: 02/06/2017
https://firqatunnajia.com/22-iogopeni-mipaka-ya-allaah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)