Rabiy´ al-Aakhir mwaka wa 02 Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) mwenyewe akashiriki katika msafara wa kijeshi wa kwenda Buwaat. Katika kipindi hicho alimuacha as-Saa-ib bin ´Uthmaan bin Madh´uun (Radhiya Allaahu ´anh) kuwa khalifa al-Madiynah. Alipofika Buwaat kupitia Radhwaa´ akarudi na hapakuwepo vita.

  • Mhusika: Imaam Ismaa´iyl bin Kathiyr ad-Dimashqiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Fusuwl fiy Siyrat-ir-Rasuwl, uk. 42-43
  • Imechapishwa: 25/04/2018