Nijuavyo ni kuwa wale wenye kujuzusha mwanaume kumwangalia mwanamke ajinabi na mikono yake hawana dalili kutoka katika Qur-aan na Sunnah isipokuwa zifuatazo:
1- Kauli ya Allaah (Ta´ala):
وَلَا يُبْدِينَ زِينَتَهُنَّ إِلَّا لِبُعُولَتِهِنَّ
“… na wala wasidhihirishe mapambo yao isipokuwa yale yanayodhihirika [kwa kuwa hakuna njia ya kuyaficha]… “[1]
Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa) amesema:
“Bi maana uso, vitanga vya mikono na pete.”
Imepokea al-A´mash kutoka kwa Sa´iyd bin Jubayr kutoka kwake. Tafsiri ya Swahabah ni hoja kama tulivyotangulia kusema.
2- Abu Daawuud amepokea katika “as-Sunan” yake kutoka kwa ´Aiashah (Radhiya Allaahu ´anhaa) ya kwamba Asmaa´ bint Abiy Bakr (Radhiya Allaahu ´anhumaa) aliingia kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na alikuwa amevaa mavazi ya kubana ambapo Mtume akageuka na kusema:
“Ee Asmaa´! Wakati mwanamke anapobaleghe hatakiwi kuonesha chochote isipokuwa hiki na hiki” na akaashiria uso na vitanga vyake vya mikono.”[2]
3- al-Bukhaariy na wengine wamepokea kutoka kwa Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa) jinsi kaka yake al-Fadhwl alivokuwa amekaa kwenye mnyama nyuma ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wakati wa Hajj ya kuaga. Pindi mwanamke kutoka Khath´am alipokuja akaanza kumtazama na yeye [mwanamke huyo] anamtazama. Hivyo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akageuza uso wake upande mwingine[3]. Katika hili kuna dalili kuwa mwanamke alionesha uso wake.
4- al-Bukhaariy na wengine wamepokea kutoka kwa Jaabir bin ´Abdillaah (Radhiya Allaahu ´anhumaa) juu ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kuwaswalisha kwake watu swalah ya idi na akawapa mawaidha na kuwakumbusha kisha akaenda kwa wanawake akawapa mawaidha na kuwakumbusha. Akasema:
“Enyi wanawake! Toeni swadaqah! Hakika nyinyi ndio wengi Motoni.” Ndipo akasimama mmoja katika wanawake bora na alikuwa na mashavu ya kupauka… “[4]
Lau uso wake ungelikuwa hauko wazi basi mtu asingelijua ana mashavu ya kupauka.
Nijuavyo ni kwamba hizi ndio dalili kuwa inajuzu kwa mwanamke kuonesha uso wake wanaume ajinabi.
[1] 24:31
[2] Abu Daawuud (4104).
[3] al-Bukhaariy (1513) na Muslim (1334).
[4] Muslim (885).
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Hijaab, uk. 28-29
- Imechapishwa: 26/03/2017
Nijuavyo ni kuwa wale wenye kujuzusha mwanaume kumwangalia mwanamke ajinabi na mikono yake hawana dalili kutoka katika Qur-aan na Sunnah isipokuwa zifuatazo:
1- Kauli ya Allaah (Ta´ala):
وَلَا يُبْدِينَ زِينَتَهُنَّ إِلَّا لِبُعُولَتِهِنَّ
“… na wala wasidhihirishe mapambo yao isipokuwa yale yanayodhihirika [kwa kuwa hakuna njia ya kuyaficha]… “[1]
Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa) amesema:
“Bi maana uso, vitanga vya mikono na pete.”
Imepokea al-A´mash kutoka kwa Sa´iyd bin Jubayr kutoka kwake. Tafsiri ya Swahabah ni hoja kama tulivyotangulia kusema.
2- Abu Daawuud amepokea katika “as-Sunan” yake kutoka kwa ´Aiashah (Radhiya Allaahu ´anhaa) ya kwamba Asmaa´ bint Abiy Bakr (Radhiya Allaahu ´anhumaa) aliingia kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na alikuwa amevaa mavazi ya kubana ambapo Mtume akageuka na kusema:
“Ee Asmaa´! Wakati mwanamke anapobaleghe hatakiwi kuonesha chochote isipokuwa hiki na hiki” na akaashiria uso na vitanga vyake vya mikono.”[2]
3- al-Bukhaariy na wengine wamepokea kutoka kwa Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa) jinsi kaka yake al-Fadhwl alivokuwa amekaa kwenye mnyama nyuma ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wakati wa Hajj ya kuaga. Pindi mwanamke kutoka Khath´am alipokuja akaanza kumtazama na yeye [mwanamke huyo] anamtazama. Hivyo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akageuza uso wake upande mwingine[3]. Katika hili kuna dalili kuwa mwanamke alionesha uso wake.
4- al-Bukhaariy na wengine wamepokea kutoka kwa Jaabir bin ´Abdillaah (Radhiya Allaahu ´anhumaa) juu ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kuwaswalisha kwake watu swalah ya idi na akawapa mawaidha na kuwakumbusha kisha akaenda kwa wanawake akawapa mawaidha na kuwakumbusha. Akasema:
“Enyi wanawake! Toeni swadaqah! Hakika nyinyi ndio wengi Motoni.” Ndipo akasimama mmoja katika wanawake bora na alikuwa na mashavu ya kupauka… “[4]
Lau uso wake ungelikuwa hauko wazi basi mtu asingelijua ana mashavu ya kupauka.
Nijuavyo ni kwamba hizi ndio dalili kuwa inajuzu kwa mwanamke kuonesha uso wake wanaume ajinabi.
[1] 24:31
[2] Abu Daawuud (4104).
[3] al-Bukhaariy (1513) na Muslim (1334).
[4] Muslim (885).
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Hijaab, uk. 28-29
Imechapishwa: 26/03/2017
https://firqatunnajia.com/21-dalili-juu-ya-kwamba-inajuzu-kwa-mwanamke-kuonesha-uso/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)