20- Yahyaa bin ´Ammaar al-Imaam ametuhadithia: Ibn Swabaah ametuhadithia: Ishaaq ametuhadithia… ح Ibn-ul-Fadhwl az-Zaahid ametuhadithia: Muhammad bin al-Fadwhl bin Muhammad bin Ishaaq bin Khuzaymah ametuhadithia: Babu yangu ametuhadithia: al-Muqriy ametuhadithia: Baba yangu amenihadithia: Harmalah bin ´Imraan ametuhadithia: Abuu Yuunus Sulaym bin Jubayr amenihadithia: Nilimsikia Abuu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) akisoma Aayah hii:
إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُكُمْ أَن تُؤَدُّوا الْأَمَانَاتِ إِلَىٰ أَهْلِهَا وَإِذَا حَكَمْتُم بَيْنَ النَّاسِ أَن تَحْكُمُوا بِالْعَدْلِ ۚ إِنَّ اللَّـهَ نِعِمَّا يَعِظُكُم بِهِ ۗ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ سَمِيعًا بَصِيرًا
“Hakika Allaah anawaamrisheni kurudisha amana kwa wenyewe na mtakapohukumu baina ya watu mhukumu kwa uadilifu. Ni uzuri wa anayokuwaidhini nayo Allaah. Hakika Allaah ni Mwenye kusikia, Mwenye kuona.” (04:58)
Halafu akaweka kidole chake cha gumba kwenye sikio lake na kidole chake cha shahaadah kwenye jicho lake na kusema: “Hivi ndivyo nilivyomsikia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akiisoma na akaweka vidole vyake juu yavyo.”[1]
Matamshi ni ya Ibn Khuzaymah.
[1] Abuu Daawuud (4728), Ibn Khuzaymah katika ”Kitaab-ut-Tawhiyd”, uk. 42-43, Ibn Hibbaan (265), al-Haakim (1/24) na al-Laalakaa’iy (688).
- Mhusika: Imaam Abu Ismaa´iyl ´Abdullaah bin Muhammad al-Answaariy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Arba´uun fiy Dalaa-il-it-Tawhiyd, uk. 46
- Imechapishwa: 25/01/2017
20- Yahyaa bin ´Ammaar al-Imaam ametuhadithia: Ibn Swabaah ametuhadithia: Ishaaq ametuhadithia… ح Ibn-ul-Fadhwl az-Zaahid ametuhadithia: Muhammad bin al-Fadwhl bin Muhammad bin Ishaaq bin Khuzaymah ametuhadithia: Babu yangu ametuhadithia: al-Muqriy ametuhadithia: Baba yangu amenihadithia: Harmalah bin ´Imraan ametuhadithia: Abuu Yuunus Sulaym bin Jubayr amenihadithia: Nilimsikia Abuu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) akisoma Aayah hii:
إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُكُمْ أَن تُؤَدُّوا الْأَمَانَاتِ إِلَىٰ أَهْلِهَا وَإِذَا حَكَمْتُم بَيْنَ النَّاسِ أَن تَحْكُمُوا بِالْعَدْلِ ۚ إِنَّ اللَّـهَ نِعِمَّا يَعِظُكُم بِهِ ۗ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ سَمِيعًا بَصِيرًا
“Hakika Allaah anawaamrisheni kurudisha amana kwa wenyewe na mtakapohukumu baina ya watu mhukumu kwa uadilifu. Ni uzuri wa anayokuwaidhini nayo Allaah. Hakika Allaah ni Mwenye kusikia, Mwenye kuona.” (04:58)
Halafu akaweka kidole chake cha gumba kwenye sikio lake na kidole chake cha shahaadah kwenye jicho lake na kusema: “Hivi ndivyo nilivyomsikia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akiisoma na akaweka vidole vyake juu yavyo.”[1]
Matamshi ni ya Ibn Khuzaymah.
[1] Abuu Daawuud (4728), Ibn Khuzaymah katika ”Kitaab-ut-Tawhiyd”, uk. 42-43, Ibn Hibbaan (265), al-Haakim (1/24) na al-Laalakaa’iy (688).
Mhusika: Imaam Abu Ismaa´iyl ´Abdullaah bin Muhammad al-Answaariy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Arba´uun fiy Dalaa-il-it-Tawhiyd, uk. 46
Imechapishwa: 25/01/2017
https://firqatunnajia.com/20-dalili-ya-kusikia-na-kuona-kwa-allaah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)