Mlango wa tatu: Mambo yanayopendekezwa ya swawm na machukizo yake. Ndani yake kuna masuala mawili:
Suala la kwanza: Mapendekezo ya funga
Imependekezwa kwa mfungaji kuchunga mambo yafuatayo:
1- Daku. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Kuleni daku. Kwani hakika katika daku kuna baraka.”[1]
Daku inapatikana kwa chakula kingi au kidogo ijapo kwa glasi ya maji. Wakati wa daku ni kuanzia nusu ya usku mpaka pale inapochomoza alfajiri.
2- Kuchelewesha daku. Zayd bin Thaabit (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza:
“Tulikula daku pamoja na Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kisha tukasimama kuswali.” Nikasema: “Kulikuwa muda kiasi gani baina yake?” Akasema: “Aayah khamsini.”[2]
3- Kuharakisha kukata swawm. Inapendekezwa kwa mfungaji kuharakisha kukata swawm pale tu ambapo atakuwa na uhakika kwamba jua limekwishazama. Sahl bin Sa´d (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Watu hawatoacha kuwa juu ya kheri muda wa kuwa wanaharakisha kukata swawm.”[3]
4- Kukata swawm kwa tende tosa, asipopata basi tende za kawaida, asipopata basi kwa glasi ya maji. Anas (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza:
“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akifuturu kwa tende tosa kabla ya kuswali. Isipokuwa tende tosa basi tende za kawaida. Isipokuwa tende za kawaida basi glasi ya maji.”[4]
Asipopata kitu basi anuie kufungua kwa moyo wake na itamtosha kufanya hivo.
5- Kuomba du´aa wakati wa kukata swawm na kipindi cha swawm. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Watu aina tatu hayarudishwi nyuma maombi yao; mfungaji mpaka akate swawm, kiongozi mwadilifu na mdhulumiwa.”[5]
6- Kukithirisha kutoa swadaqah, kusoma Qur-aan, kuwafuturisha wafungaji na matendo mema mengine. Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa) ameeleza:
“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa ni mkarimu zaidi wa watu. Ramadhaan alikuwa mkarimu zaidi wakati anapokutana na Jibriyl. Jibriyl alikuwa akikutana naye katika kila usiku wa Ramadhaan ambapo anamfunza Qur-aan. Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wakati anapokutana na Jibriyl basi anakuwa ni mkarimu zaidi katika mambo ya kheri kuliko upepo ulioagizwa.”[6]
7- Kujitahidi swalah ya usiku na khaswa katika zile siku kumi za Ramadhaan. ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) ameeleza:
“Zinapoingia zile kumi basi anafunga vizuri kikoi chake, anauhuisha usiku wake na anawaamsha familia yake.”[7]
Pia kutokana na kuenea kwa maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Yule mwenye kufunga Ramadhaan kwa imani na kwa matarajio basi atasamehewa dhambi zake zilizotangulia.”[8]
8- Kufanya ´Umrah. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Kufanya ´Umrah katika Ramadhaan ni sawa na hijjah.”[9]
9- Kusema “Mimi nimefunga” kumwambia yule mwenye kumtukana. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Itapokuwa ni siku ya funga ya mmoja wenu, basi asizungumze maneno machafu wala asipige kelele. Mtu akimtukana au akamgombeza, basi amwambie: “Mimi ni mtu nimefunga.”[10]
[1] al-Bukhaariy (1923) na Muslim (1095).
[2] al-Bukhaariy (575) na Muslim (1097).
[3]al-Bukhaariy (1957) na Muslim (1098).
[4] Abu Daawuud (2356) na at-Tirmidhiy (696) ambaye ameifanya kuwa nzuri.
[5] at-Tirmidhiy (2526) ambaye ameifanya kuwa nzuri na al-Bayahqiy (03/345).
[6] al-Bukhaariy (06) na Muslim (2308).
[7] al-Bukhaariy (2024) na Muslim (1174).
[8] Muslim (759).
[9] al-Bukhaariy (1782) na Muslim (1256).
[10] al-Bukhaariy (1904) na Muslim (1151).
- Mhusika: Nukhbatin minal-´Ulamaa´
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fiqh-ul-Muyassar, uk. 159-160
- Imechapishwa: 26/04/2020
Mlango wa tatu: Mambo yanayopendekezwa ya swawm na machukizo yake. Ndani yake kuna masuala mawili:
Suala la kwanza: Mapendekezo ya funga
Imependekezwa kwa mfungaji kuchunga mambo yafuatayo:
1- Daku. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Kuleni daku. Kwani hakika katika daku kuna baraka.”[1]
Daku inapatikana kwa chakula kingi au kidogo ijapo kwa glasi ya maji. Wakati wa daku ni kuanzia nusu ya usku mpaka pale inapochomoza alfajiri.
2- Kuchelewesha daku. Zayd bin Thaabit (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza:
“Tulikula daku pamoja na Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kisha tukasimama kuswali.” Nikasema: “Kulikuwa muda kiasi gani baina yake?” Akasema: “Aayah khamsini.”[2]
3- Kuharakisha kukata swawm. Inapendekezwa kwa mfungaji kuharakisha kukata swawm pale tu ambapo atakuwa na uhakika kwamba jua limekwishazama. Sahl bin Sa´d (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Watu hawatoacha kuwa juu ya kheri muda wa kuwa wanaharakisha kukata swawm.”[3]
4- Kukata swawm kwa tende tosa, asipopata basi tende za kawaida, asipopata basi kwa glasi ya maji. Anas (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza:
“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akifuturu kwa tende tosa kabla ya kuswali. Isipokuwa tende tosa basi tende za kawaida. Isipokuwa tende za kawaida basi glasi ya maji.”[4]
Asipopata kitu basi anuie kufungua kwa moyo wake na itamtosha kufanya hivo.
5- Kuomba du´aa wakati wa kukata swawm na kipindi cha swawm. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Watu aina tatu hayarudishwi nyuma maombi yao; mfungaji mpaka akate swawm, kiongozi mwadilifu na mdhulumiwa.”[5]
6- Kukithirisha kutoa swadaqah, kusoma Qur-aan, kuwafuturisha wafungaji na matendo mema mengine. Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa) ameeleza:
“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa ni mkarimu zaidi wa watu. Ramadhaan alikuwa mkarimu zaidi wakati anapokutana na Jibriyl. Jibriyl alikuwa akikutana naye katika kila usiku wa Ramadhaan ambapo anamfunza Qur-aan. Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wakati anapokutana na Jibriyl basi anakuwa ni mkarimu zaidi katika mambo ya kheri kuliko upepo ulioagizwa.”[6]
7- Kujitahidi swalah ya usiku na khaswa katika zile siku kumi za Ramadhaan. ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) ameeleza:
“Zinapoingia zile kumi basi anafunga vizuri kikoi chake, anauhuisha usiku wake na anawaamsha familia yake.”[7]
Pia kutokana na kuenea kwa maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Yule mwenye kufunga Ramadhaan kwa imani na kwa matarajio basi atasamehewa dhambi zake zilizotangulia.”[8]
8- Kufanya ´Umrah. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Kufanya ´Umrah katika Ramadhaan ni sawa na hijjah.”[9]
9- Kusema “Mimi nimefunga” kumwambia yule mwenye kumtukana. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Itapokuwa ni siku ya funga ya mmoja wenu, basi asizungumze maneno machafu wala asipige kelele. Mtu akimtukana au akamgombeza, basi amwambie: “Mimi ni mtu nimefunga.”[10]
[1] al-Bukhaariy (1923) na Muslim (1095).
[2] al-Bukhaariy (575) na Muslim (1097).
[3]al-Bukhaariy (1957) na Muslim (1098).
[4] Abu Daawuud (2356) na at-Tirmidhiy (696) ambaye ameifanya kuwa nzuri.
[5] at-Tirmidhiy (2526) ambaye ameifanya kuwa nzuri na al-Bayahqiy (03/345).
[6] al-Bukhaariy (06) na Muslim (2308).
[7] al-Bukhaariy (2024) na Muslim (1174).
[8] Muslim (759).
[9] al-Bukhaariy (1782) na Muslim (1256).
[10] al-Bukhaariy (1904) na Muslim (1151).
Mhusika: Nukhbatin minal-´Ulamaa´
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fiqh-ul-Muyassar, uk. 159-160
Imechapishwa: 26/04/2020
https://firqatunnajia.com/19-yaliyopendekezwa-kwa-mfungaji/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)