19. Kuna wajibu upi juu ya Maswahabah wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)?

Swali 19: Kuna wajibu upi juu ya Maswahabah wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)?

Jibu: Katika utimilifu wa kumuamini na kumpenda Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni kuwapenda Maswahabah zake kutokamana daraja na kutangulia kwao.

Mtu anatakiwa kukiri fadhila zao ambazo wamewashinda kwazo Ummah mzima.

Mtu anatakiwa kumuabudu Allaah kwa kuwapenda na kueneza fadhila zao.

Haifai kwa mtu kuingilia yale yaliyopitika kati yao.

Ni lazima kwetu kuamini kuwa wao wana haki zaidi ya kila sifa yenye kusifiwa kuliko walivyo wengine na kwamba wao wamewatangulia wengine wote katika kila kheri na wako mbali kabisa na kila shari.

Ni lazima kuamini kuwa wote walikuwa ni waadilifu na kwamba Allaah amewaridhia.

  • Mfasiri: Firqatunnajia.com