Halafu (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akamtuma ami yake Hamzah (Radhiya Allaahu ´anh) kwenda pwani. Alikuwa pamoja naye wapandaji thelathini na hakukuwemo na Answaar hata mmoja. Huko wakakutana na Abu Jahl bin Hishaam na alikuwa na msafara wa watu takriban 300. Majdiy bin ´Amr al-Juhaniy akaingilia kati yao kwa sababu alikuwa na mkataba wa amani na pande zote mbili.

  • Mhusika: Imaam Ismaa´iyl bin Kathiyr ad-Dimashqiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Fusuwl fiy Siyrat-ir-Rasuwl, uk. 41
  • Imechapishwa: 25/04/2018