18. Ni haki zepi walizo nazo waislamu juu yako?

Swali 18: Ni haki zepi ambazo waislamu wako nazo juu yako?

Jibu: Allaah (Ta´ala) amesema:

إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ إِخْوَةٌ

“Hakika waumini ni ndugu.” (49:10)

Ni wajibu kuwafanya kama ndugu. Wapendelee kile unachojipendelea juu ya nafsi yako na uwachukilie kile unachojichukilia juu ya nafsi yako. Unatakiwa kujitahidi kiasi na unavyoweza juu ya manufaa yao na kuhakikisha uhusiano wao ni mzuri na kwamba ni wamoja na wakusanyike juu ya haki.

Muislamu ni ndugu wa muislamu mwenzie; hamdhulumu, hamdharau, hamdanganyi na wala hamwaibishi.

Aidha unatakiwa kuwapa haki maalum wenye kukuhusu kama wazazi, jamaa, majirani, marafiki na wafanyakazi wenzio.

  • Mfasiri: Firqatunnajia.com