Swali 18: Ni ipi hukumu ya kuzuia uzazi kutokana na sababu za kimatibabu za sasa na zitazokuja huko baadaye, kama wanavyotarajia mamlaka ya kimatibabu na ya kisayansi?

Jibu: Ikiwa kuna dharurah hakuna neno. Vinginevyo kilicho cha wajibu ni kuacha kufanya hivo. Kwa sababu Shari´ah inapendekeza kizazi na inaita katika sababu zake kwa ajili ya kuufanya Ummah kuwa mkubwa. Lakini kukiwa kuna dharurah hakuna neno. Ni kama ambavyo inafaa kutumia uzazi wa mpango kwa muda mfupi kwa ajili ya manufaa ya Kishari´ah.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Ahkaam Swalaat-il-Mariydhw, uk. 41
  • Imechapishwa: 03/08/2019