Kuamini Qadar ni katika misingi ya imani. Imethibiti katika Hadiyth ya Jibriyl ambapo alimuuliza Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amweleze kuhusu imani. Akasema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Imani ni kumuamini Allaah, Malaika Wake, Vitabu Vyake, Mitume Yake, siku ya Mwisho na kuamini Qadar kheri na shari yake.”[1]
Amesema (Ta´ala):
إِنَّا كُلَّ شَيْءٍ خَلَقْنَاهُ بِقَدَرٍ
“Hakika sisi Tumekiumba kila kitu kwa makadirio.”[2]
Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Pupia yale yenye kukunufaisha na utake msaada kwa Allaah. Ikiwa utafikwa na kitu basi usisemi “lau ningefanya kadhaa ingelikuwa kadhaa”. Badala yake unatakiwa useme: “Amekadiria Allaah na akitakacho huwa.” Kwani hakika ya “lau…” inafungua matendo ya shaytwaan.”[3]
Hadiyth na maandiko juu ya haya ni mengi. Msingi huu ni wenye kujulikana. Haki ndani yake inajulikana. ´Aqiydah ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah juu yake iko wazi. ´Aqiydah yao imejengwa juu ya yale yaliyokuja katika Qur-aan na Sunnah. Kuhusu wale waliopinda na msingi huu hilo limetokamana na kufuata nafsi zao na matamanio yao na wakati huohuo wakaipa mgongo Qur-aan na Sunnah. Hali inakuwa namna hii kwa kila ambaye anajaribu kutoka nje ya dalili za Qur-aan na Sunnah. Natija yake hutumbukia katika upotevu. Amesema (Ta´ala):
وَأَنَّ هَـٰذَا صِرَاطِي مُسْتَقِيمًا فَاتَّبِعُوهُ ۖ وَلَا تَتَّبِعُوا السُّبُلَ فَتَفَرَّقَ بِكُمْ عَن سَبِيلِهِ
“Na kwamba hii njia Yangu iliyonyooka – hivyo basi, ifuateni – na wala msifuate vijia vya vichochoro vikakufarikisheni na njia Yake.”[4]
[1] al-Bukhaariy (4499), Muslim (10), an-Nasaa´iy (4991), Ibn Maajah (64) na Ahmad (02/426).
[2] 54:49
[3] Muslim (2664), Ibn Maajah (79) na Ahmad (02/370).
[4] 06:153
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Mujmal ´Aqiydat-is-Salaf as-Swaalih, uk. 16
- Imechapishwa: 24/05/2022
Kuamini Qadar ni katika misingi ya imani. Imethibiti katika Hadiyth ya Jibriyl ambapo alimuuliza Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amweleze kuhusu imani. Akasema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Imani ni kumuamini Allaah, Malaika Wake, Vitabu Vyake, Mitume Yake, siku ya Mwisho na kuamini Qadar kheri na shari yake.”[1]
Amesema (Ta´ala):
إِنَّا كُلَّ شَيْءٍ خَلَقْنَاهُ بِقَدَرٍ
“Hakika sisi Tumekiumba kila kitu kwa makadirio.”[2]
Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Pupia yale yenye kukunufaisha na utake msaada kwa Allaah. Ikiwa utafikwa na kitu basi usisemi “lau ningefanya kadhaa ingelikuwa kadhaa”. Badala yake unatakiwa useme: “Amekadiria Allaah na akitakacho huwa.” Kwani hakika ya “lau…” inafungua matendo ya shaytwaan.”[3]
Hadiyth na maandiko juu ya haya ni mengi. Msingi huu ni wenye kujulikana. Haki ndani yake inajulikana. ´Aqiydah ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah juu yake iko wazi. ´Aqiydah yao imejengwa juu ya yale yaliyokuja katika Qur-aan na Sunnah. Kuhusu wale waliopinda na msingi huu hilo limetokamana na kufuata nafsi zao na matamanio yao na wakati huohuo wakaipa mgongo Qur-aan na Sunnah. Hali inakuwa namna hii kwa kila ambaye anajaribu kutoka nje ya dalili za Qur-aan na Sunnah. Natija yake hutumbukia katika upotevu. Amesema (Ta´ala):
وَأَنَّ هَـٰذَا صِرَاطِي مُسْتَقِيمًا فَاتَّبِعُوهُ ۖ وَلَا تَتَّبِعُوا السُّبُلَ فَتَفَرَّقَ بِكُمْ عَن سَبِيلِهِ
“Na kwamba hii njia Yangu iliyonyooka – hivyo basi, ifuateni – na wala msifuate vijia vya vichochoro vikakufarikisheni na njia Yake.”[4]
[1] al-Bukhaariy (4499), Muslim (10), an-Nasaa´iy (4991), Ibn Maajah (64) na Ahmad (02/426).
[2] 54:49
[3] Muslim (2664), Ibn Maajah (79) na Ahmad (02/370).
[4] 06:153
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Mujmal ´Aqiydat-is-Salaf as-Swaalih, uk. 16
Imechapishwa: 24/05/2022
https://firqatunnajia.com/18-hii-ndio-sababu-ya-waliopinda-katika-qadar/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)