18. Fuata Qur-aan na Sunnah kwa ufahamu wa Salaf

Dini itaendelea yenye kubaki mpaka kifike Qiyaamah. Dini haibadiliki kwa kubadilika kwa zama. Dini ni yenye kutumika katika kila zama na kila mahali. Chenye kubadilika ni mambo ya Ijtihaad ya kiuanaadamu. Kuhusu dini haibadiliki. Dini ni yenye kutumika katika kila zama na mahali. Kwa sababu ni yenye kutoka kwa Allaah. Kwa ajili hiyo ndi maana wamependekeza – wanachuoni – kusema:

“Shikamaneni na Qur-aan na Sunnah kwa ufahamu wa as-Salaf as-Swaalih.”

Usizue uelewa wako wenyewe au kutoka kwa waliokuja nyuma.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Sharh-is-Sunnah, uk. 44
  • Imechapishwa: 08/12/2017