178. Eda ya mwanamke baada ya mwaka mmoja

Swali 178: Swali lililojumuishwa ambalo linauliza hukumu ya suala la mwanamke ambaye amefiwa na mume wake na hakumkalia eda isipokuwa baada ya kupita mwaka mmoja tangu kufariki kwake[1]?

Jibu: Ni lazima kwa mwanamke kukaa eda na kuacha mapambo moja kwa moja baada ya kufiwa na mume wake; miezi minne na siku kumi akiwa si mjamzito. Akiwa ni mjamzito anatakiwa kukaa eda mpaka pale atakapojifungua. Akiwa hajui kifo cha mume wake isipokuwa baada ya kupita kitambo kirefu basi hakumlazimu kukaa eda wala kuacha mapambo. Kwa sababu kipindi chake kimekwishapita. Haijuzu kwa mwanamke kuizingatia nafsi yake kuwa yuko ndani ya eda au kuacha mapambo baada ya kupita kitambo. Akiwa ni mjinga basi afunzwe na abainishiwe hukumu ya ki-Shari´ah. Kwa sababu watu wengi wanajahili hukumu za Shari´ah. Tunamwomba Allaah atutunuku sisi na nyinyi na waislamu wote uelewa katika dini na uthabiti juu yake.

[1] Majmuu´-ul-Fataawaa (22/227-228).

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Ahkaam-ul-Janaa-iz, uk. 133-134
  • Imechapishwa: 10/02/2022