“Kichwa cha khabari kingine cha uchokozi ulichoandika ni: “Qawl Sayyid Qutwub bi Wahdat-il-Wujuud[1]“. Sayyid (Rahimahu Allaah) amezungumza maneno yasiyokuwa ya wazi, usulubu mzito alipokuwa akifasiri Suurah “al-Hadiyd” na “al-Ikhlaasw”. Yametumiwa katika kumnasibishia nadharia ya kwamba viumbe vyote ni Allaah. Umefanya vizuri uliponukuu radd yake kwa nadharia ya viumbe vyote ni Allaah katika tafsiri ya “al-Baqarah”. Katika hayo ni pamoja na maneno yake: “Kuanzia hapa nadharia ya viumbe vyote ni Allaah imeisha kutokamana na fikira ya Kiislamu sahihi.””

1- Si mimi peke yangu niliyesema kuwa Sayyid Qutwub amezungumza kwa nadharia ya kwamba viumbe vyote ni Allaah. Kuna wanachuoni wengine waliosema hivo kama Shaykh Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy.

2- Maneno yake juu ya nadharia yenye kusema viumbe vyote ni Allaah katika tafsiri ya Suurah mbili zilizotajwa yako wazi kabisa na sio maneno yenye kutatiza. Kwa mfano katika tafsiri ya “al-Hadiyd” anasema:

“Mtu anakaribia kutowahi kufikiria uhakika huu mkubwa unaojaza mazingira ya kiuanaadamu kabla ya mtu kuona uhakika mwingine ambao huenda ndio mkubwa na wenye nguvu zaidi, nao ni mazingira ya uhakika wa uwepo. Kwa hiyo mazingira pekee ya kweli kabisa ni mazingira ya Allaah (Subaanahu wa Ta´ala).”

Haya yako wazi kabisa anazungumza kwa nadharia ya kwamba viumbe wote ni Allaah. Isitoshe amesema katika tafsiri hiyo hiyo:

“Vitu vyote havina uhakika wala uwepo. Haya hata vilevile ule moyo unaopata tu kuchukua sehemu ya ule uhakika Mkubwa.”

Hii ni nadharia ilio wazi kabisa ya kwamba viumbe wote ni Allaah kuliko maneno ya baadhi ya watu wenye nadharia hii:

“Uwepo ni mionzi ya kidhati ya Muumba.”

Vilevile amesema:

“Pindi mtazamo huu, usiyoona uwepo wa yeyote isipokuwa uhakika wa Allaah, utapokita, unaongozana. Katika awamu hii mkono wa Allaah unaona kila kile inachoona. Baada ya hapo kunakuja awamu nyingine ambapo mtu haoni kitu kingine katika ulimwengu isipokuwa Allaah tu kwa sababu uhalisia ni kwamba hakuna uhakika wa yeyote ambao mtu anaona isipokuwa uhakika wa Allaah.”

[1] Sayyid Qutwub anazungumza kwa nadharia ya kwamba viumbe vyote ni Allaah.