Imesemekana kuwa Qadariyyah ni waabudia moto wa Ummah huu. Kwa nini? Kwa sababu wamethibitisha kuwepo waungu wawili pamoja na Allaah. Wanaonelea kuwa kila mtu anaumba matendo yake mwenyewe. Kwa ajili hiyo ndio maana wakapotea na wakawa ni wenye kustahiki chuki na kusimangwa na Ahl-ul-Haqq. Hili si kwa jengine ni kwa sababu wamekosea katika msingi huu mkubwa ambao ni kuamini Qadar.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Mujmal ´Aqiydat-is-Salaf as-Swaalih, uk. 15
  • Imechapishwa: 24/05/2022