Swali 17: Ni ipi hukumu ya ambaye aliacha kulipa swawm ya Ramadhaan mpaka akaingiliwa na Ramadhaan ilio baada yake ilihali hakuwa na udhuru? Je, inatosha kwake kutubia pamoja na kulipa au ni lazima vilevile kutoa kafara?
Jibu: Ni lazima kwake kutubia kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) na kulisha masikini kwa kila siku moja aliyoacha pamoja na kulipa funga. Kafara ni nusu ya pishi kwa kipimo cha ile pishi ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa kile chakula kilichozoeleka kuliwa katika nchi kama mfano wa tende, ngano, mchele au vyenginevyo. Kiwango chake ni 1,5 kg kwa njia ya kukadiria. Hana kafara nyingine zaidi ya hiyo. Hivo ndivo walivyofutu baadhi ya Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) akiwemo Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa).
Lakini kama alikuwa na udhuru kwa mfano mgonjwa au msafiri au mwanamke alikuwa na udhuru kama mfano wa ujauzito au kunyonyesha ambapo angelifunga basi angelihisi uzito, hakuna kinachomlazimu zaidi ya kulipa.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdllaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: As-ilah Muhimmah tata´alaqah bisw-Swiyaam, uk. 23-24
- Imechapishwa: 29/04/2019
Swali 17: Ni ipi hukumu ya ambaye aliacha kulipa swawm ya Ramadhaan mpaka akaingiliwa na Ramadhaan ilio baada yake ilihali hakuwa na udhuru? Je, inatosha kwake kutubia pamoja na kulipa au ni lazima vilevile kutoa kafara?
Jibu: Ni lazima kwake kutubia kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) na kulisha masikini kwa kila siku moja aliyoacha pamoja na kulipa funga. Kafara ni nusu ya pishi kwa kipimo cha ile pishi ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa kile chakula kilichozoeleka kuliwa katika nchi kama mfano wa tende, ngano, mchele au vyenginevyo. Kiwango chake ni 1,5 kg kwa njia ya kukadiria. Hana kafara nyingine zaidi ya hiyo. Hivo ndivo walivyofutu baadhi ya Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) akiwemo Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa).
Lakini kama alikuwa na udhuru kwa mfano mgonjwa au msafiri au mwanamke alikuwa na udhuru kama mfano wa ujauzito au kunyonyesha ambapo angelifunga basi angelihisi uzito, hakuna kinachomlazimu zaidi ya kulipa.
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdllaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: As-ilah Muhimmah tata´alaqah bisw-Swiyaam, uk. 23-24
Imechapishwa: 29/04/2019
https://firqatunnajia.com/17-ni-ipi-hukumu-ya-aliyechelewesha-kulipa-mpaka-akaingiliwa-na-ramadhaan-nyingine/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)