Majina yaliyopendekezwa na kujuzu yamegawanyika katika ngazi mbalimbali na yako kama ifuatavyo:
1- Imependekezwa kumpa mvulana jina la “´Abdullaah”, mja wa Allaah, au “´Abdur-Rahmaan”, mja wa Mwingi wa rehema. Hayo ndio majina yanayopendwa zaidi na Allaah (Ta´ala), kama ilivyothibiti ikiwa ni pamoja vilevile na Muslim na Abu Daawuud kupitia kwa Ibn ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa) kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Majina hayo mawili yanathibitisha uja ambao ndio uhakika wa mwanaadamu. Allaah ametaja tu majina hayo mawili pindi alipokuwa akitilia mkazo uja wa mwanaadamu. Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) amesema:
وَأَنَّهُ لَمَّا قَامَ عَبْدُ اللَّـهِ يَدْعُوهُ كَادُوا يَكُونُونَ عَلَيْهِ لِبَدًا
“Pindi mja wa Allaah aliposimama kumwomba walikaribia kumzonga [kama vile wanataka kumwacha].” (72:19)
وَعِبَادُ الرَّحْمَـٰنِ الَّذِينَ يَمْشُونَ عَلَى الْأَرْضِ هَوْنًا
“Waja wa Mwingi wa Rahmah ni wale wanaotembea katika ardhi kwa unyenyekevu.” (25:63)
قُلِ ادْعُوا اللَّـهَ أَوِ ادْعُوا الرَّحْمَـٰنَ ۖأَيًّا مَّا تَدْعُوا فَلَهُ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ
“Sema: “Muiteni Allaah au muiteni Mwingi wa Rahmah! Vyovyote mtakavyomwita [bado ni Yule Yule Mmoja], Yeye ana majina Mazuri kabisa.” (17:110)
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimpa binadamu yake jina la “´Abdullaah” (Radhiya Allaahu ´anh).
Kulikuwa takriban Maswahabah 300 wakiitwa “´Abdullaah”. Mtoto wa kwanza wa Muhaajiruun aliyezaliwa alipewa jina la “´Abdullaah”, naye ni ´Abdullaah bin az-Zubayr (Radhiya Allaahu ´anhum).
- Mhusika: ´Allaamah Bakr bin ´Abdillaah Abu Zayd
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Tasmiyat-ul-Mawluwd, uk. 16
- Imechapishwa: 18/03/2017
Majina yaliyopendekezwa na kujuzu yamegawanyika katika ngazi mbalimbali na yako kama ifuatavyo:
1- Imependekezwa kumpa mvulana jina la “´Abdullaah”, mja wa Allaah, au “´Abdur-Rahmaan”, mja wa Mwingi wa rehema. Hayo ndio majina yanayopendwa zaidi na Allaah (Ta´ala), kama ilivyothibiti ikiwa ni pamoja vilevile na Muslim na Abu Daawuud kupitia kwa Ibn ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa) kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Majina hayo mawili yanathibitisha uja ambao ndio uhakika wa mwanaadamu. Allaah ametaja tu majina hayo mawili pindi alipokuwa akitilia mkazo uja wa mwanaadamu. Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) amesema:
وَأَنَّهُ لَمَّا قَامَ عَبْدُ اللَّـهِ يَدْعُوهُ كَادُوا يَكُونُونَ عَلَيْهِ لِبَدًا
“Pindi mja wa Allaah aliposimama kumwomba walikaribia kumzonga [kama vile wanataka kumwacha].” (72:19)
وَعِبَادُ الرَّحْمَـٰنِ الَّذِينَ يَمْشُونَ عَلَى الْأَرْضِ هَوْنًا
“Waja wa Mwingi wa Rahmah ni wale wanaotembea katika ardhi kwa unyenyekevu.” (25:63)
قُلِ ادْعُوا اللَّـهَ أَوِ ادْعُوا الرَّحْمَـٰنَ ۖأَيًّا مَّا تَدْعُوا فَلَهُ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ
“Sema: “Muiteni Allaah au muiteni Mwingi wa Rahmah! Vyovyote mtakavyomwita [bado ni Yule Yule Mmoja], Yeye ana majina Mazuri kabisa.” (17:110)
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimpa binadamu yake jina la “´Abdullaah” (Radhiya Allaahu ´anh).
Kulikuwa takriban Maswahabah 300 wakiitwa “´Abdullaah”. Mtoto wa kwanza wa Muhaajiruun aliyezaliwa alipewa jina la “´Abdullaah”, naye ni ´Abdullaah bin az-Zubayr (Radhiya Allaahu ´anhum).
Mhusika: ´Allaamah Bakr bin ´Abdillaah Abu Zayd
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Tasmiyat-ul-Mawluwd, uk. 16
Imechapishwa: 18/03/2017
https://firqatunnajia.com/17-majina-mawili-yanayopendwa-zaidi-na-allaah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)