17. Hadiyth “Allaah (Tabaarak wa Ta´ala) aliwapoteza wale waliokuwa kabla yetu siku ya ijumaa.. “

699- Abu Hurayrah na Hudhayfah (Radhiya Allaahu ´anhumaa) wameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

”Allaah (Tabaarak wa Ta´ala) aliwapoteza wale waliokuwa kabla yetu siku ya ijumaa. Mayahudi walikuwa na siku ya jumamosi na manaswara siku ya jumapili. Wao ni wenye kufuata mpaka siku ya Qiyaamah. Sisi ni wa mwisho katika dunia hii na wa kwanza siku ya Qiyaamah ambao tutahukumiwa kabla ya viumbe wengine wote.”[1]

Ameipokea Ibn Maajah na al-Bazzaar. Wapokezi wake ni Swahiyh. Hata hivyo al-Bazzaar amesema:

Sisi ni wa mwisho katika dunia hii na wa kwanza siku ya Qiyaamah ambao tutasamehewa kabla ya viumbe wengine wote.”

[1] Swahiyh.

  • Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/437)
  • Imechapishwa: 13/01/2018