Ramadhaan ilifaradhishwa mwaka wa pili baada ya kuhajiri ambapo Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akafunga miaka tisa. Kufunga kulipitia hatua mbili:
1- Hatua ya kwanza mtu alikuwa na chaguo kati ya kufunga na kulisha pamoja na kwamba kufunga ndio ilikuwa bora zaidi.
2- Hatua ya pili ilikuwa ulazima wa kufunga bila ya mtu kuwa na chaguo. al-Bukhaariy na Muslim wamepotea kupitia kwa Salamah non al-Akwaa´ (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kwamba kulipoteremka:
وَعَلَى الَّذِينَ يُطِيقُونَهُ فِدْيَةٌ طَعَامُ مِسْكِينٍ
“Na ni juu ya wale wanaoiweza [kufunga swawm] lakini kwa tabu watoe fidia kulisha masikini.”
Alikuwa anayetaka kula na kutoa fidia anafanya hivo. Hali iliendelea hivo mpaka kuliposhuka Aayah iliobaada yake ambapo ikaifuta. Nayo ni maneno Yake (Ta´ala):
فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ ۖ وَمَن كَانَ مَرِيضًا أَوْ عَلَىٰ سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ
“Basi atakayeshuhudia miongoni mwenu mwezi [mpya] na afunge swawm. Na atakayekuwa mgonjwa au safarini basi [atimize] idadi katika siku nyinginezo.”[1]
Hapo ndipo Allaah akatuwajibishia kufunga bila ya kuwa na chaguo jengine.
Hailazimiki kufunga mpaka kuthibiti kuingia kwa mwezi. Mtu asifunge kabla ya kuingia kwa mwezi. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mmoja wetu asiitangulizie Ramadhaan kwa kufunga siku moja au siku mbili; isipokuwa mtu ambaye alikuwa na mazowea ya kufunga basi aendelee kufunga siku hiyo.”
Ameipokea al-Bukhaariy.
[1] 02:183
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majaalis Shahr Ramadhwaan, uk. 19-21
- Imechapishwa: 10/04/2020
Ramadhaan ilifaradhishwa mwaka wa pili baada ya kuhajiri ambapo Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akafunga miaka tisa. Kufunga kulipitia hatua mbili:
1- Hatua ya kwanza mtu alikuwa na chaguo kati ya kufunga na kulisha pamoja na kwamba kufunga ndio ilikuwa bora zaidi.
2- Hatua ya pili ilikuwa ulazima wa kufunga bila ya mtu kuwa na chaguo. al-Bukhaariy na Muslim wamepotea kupitia kwa Salamah non al-Akwaa´ (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kwamba kulipoteremka:
وَعَلَى الَّذِينَ يُطِيقُونَهُ فِدْيَةٌ طَعَامُ مِسْكِينٍ
“Na ni juu ya wale wanaoiweza [kufunga swawm] lakini kwa tabu watoe fidia kulisha masikini.”
Alikuwa anayetaka kula na kutoa fidia anafanya hivo. Hali iliendelea hivo mpaka kuliposhuka Aayah iliobaada yake ambapo ikaifuta. Nayo ni maneno Yake (Ta´ala):
فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ ۖ وَمَن كَانَ مَرِيضًا أَوْ عَلَىٰ سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ
“Basi atakayeshuhudia miongoni mwenu mwezi [mpya] na afunge swawm. Na atakayekuwa mgonjwa au safarini basi [atimize] idadi katika siku nyinginezo.”[1]
Hapo ndipo Allaah akatuwajibishia kufunga bila ya kuwa na chaguo jengine.
Hailazimiki kufunga mpaka kuthibiti kuingia kwa mwezi. Mtu asifunge kabla ya kuingia kwa mwezi. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mmoja wetu asiitangulizie Ramadhaan kwa kufunga siku moja au siku mbili; isipokuwa mtu ambaye alikuwa na mazowea ya kufunga basi aendelee kufunga siku hiyo.”
Ameipokea al-Bukhaariy.
[1] 02:183
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majaalis Shahr Ramadhwaan, uk. 19-21
Imechapishwa: 10/04/2020
https://firqatunnajia.com/16-ramadhaan-ilipita-katika-hatua-mbili/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)