74- Jua likishazama, ataondoka kutoka ´Arafah na kuelekea Muzdalifah kwa utulivu na upole. Asisiongamane na watu kwa mwili wake, mnyama wake wa kupanda au gari yake. Atapojipatia nafasi basi akaze mwendo.
75- Atapofika, kuadhiniwe na kukimiwe na kuswaliwe Maghrib Rak´ah tatu. Kisha kukimiwe tena na kuswaliwe ´Ishaa kwa kufupisha na kujumuishwe kati yazo.
76- Atakayetenganisha baina ya swalah hizi mbili kwa sababu ya haja hakuna neno[1].
77- Vivyo hivyo asiswali chochote baina ya swalah hizi mbili wala baada ya swalah ya ´Ishaa[2].
78- Kisha alale mpaka Fajr.
79- Itapombainikia kwamba Fajr imepambazuka, basi aswali mwanzoni mwa kuingia wakati kwa kutoa adhaana na Iqaamah.
[1] Haya ni maoni ya Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah kwa sababu hilo limethibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na Maswahabah wake, kama ilivyotajwa katika “al-Bukhaariy” (25/94/801). Tazama ”Mukhtaswar al-Bukhaariy”.
[2] Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah amesema:
“Atapofika Muzdalifah, basi ikiwezekana aswali Maghrib kabla ya ngamia hajatua magoti chini. Ngamia akishatua magoti yake chini, aswali ´Ishaa. Endapo atachelewesha ´Ishaa, basi hilo halidhuru.”
- Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Manaasik-ul-Hajj wal-´Umrah, uk. 30
- Imechapishwa: 17/07/2018
74- Jua likishazama, ataondoka kutoka ´Arafah na kuelekea Muzdalifah kwa utulivu na upole. Asisiongamane na watu kwa mwili wake, mnyama wake wa kupanda au gari yake. Atapojipatia nafasi basi akaze mwendo.
75- Atapofika, kuadhiniwe na kukimiwe na kuswaliwe Maghrib Rak´ah tatu. Kisha kukimiwe tena na kuswaliwe ´Ishaa kwa kufupisha na kujumuishwe kati yazo.
76- Atakayetenganisha baina ya swalah hizi mbili kwa sababu ya haja hakuna neno[1].
77- Vivyo hivyo asiswali chochote baina ya swalah hizi mbili wala baada ya swalah ya ´Ishaa[2].
78- Kisha alale mpaka Fajr.
79- Itapombainikia kwamba Fajr imepambazuka, basi aswali mwanzoni mwa kuingia wakati kwa kutoa adhaana na Iqaamah.
[1] Haya ni maoni ya Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah kwa sababu hilo limethibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na Maswahabah wake, kama ilivyotajwa katika “al-Bukhaariy” (25/94/801). Tazama ”Mukhtaswar al-Bukhaariy”.
[2] Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah amesema:
“Atapofika Muzdalifah, basi ikiwezekana aswali Maghrib kabla ya ngamia hajatua magoti chini. Ngamia akishatua magoti yake chini, aswali ´Ishaa. Endapo atachelewesha ´Ishaa, basi hilo halidhuru.”
Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Manaasik-ul-Hajj wal-´Umrah, uk. 30
Imechapishwa: 17/07/2018
https://firqatunnajia.com/16-kuondoka-kutoka-arafah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)