47- Ni katika adabu mtu kuashiria haja yake. Hivyo ndivyo walivyokuwa wakifanya Mitume na watu bora na mawalii waliowafuata.
48- Allaah (Ta´ala) amesema:
وَأَيُّوبَ إِذْ نَادَىٰ رَبَّهُ أَنِّي مَسَّنِيَ الضُّرُّ وَأَنتَ أَرْحَمُ الرَّاحِمِينَ
“Na Ayyuub alipomwita Mola wake [akiomba]: “Hakika mimi imenigusa dhara, Nawe ndiye mbora zaidi wa kurehemu kuliko wengine wote wenye kurehemu”. (21:83)
Aliashiria tu na hakuomba moja kwa moja. Hali kadhalika ndivyo alivyofanya Muusa wakati alipokuwa amekaa chini ya kivuli:
فَسَقَىٰ لَهُمَا ثُمَّ تَوَلَّىٰ إِلَى الظِّلِّ فَقَالَ رَبِّ إِنِّي لِمَا أَنزَلْتَ إِلَيَّ مِنْ خَيْرٍ فَقِيرٌ
“Basi akawanyweshea, kisha akageuka kwenda kivulini, akasema: “Mola wangu! Hakika mimi ni mhitajia wa kheri Utakayoniteremshia.” (28:24)
Alikuwa ni mwenye njaa alipoashiria hivyo. Na Mtume wetu (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akiangalia mbinguni akiashiria maombi. Hapo ndipo akaambiwa:
قَدْ نَرَىٰ تَقَلُّبَ وَجْهِكَ فِي السَّمَاءِ ۖ فَلَنُوَلِّيَنَّكَ قِبْلَةً تَرْضَاهَا
“Hakika Tumeona unavyogeuzageuza uso wako mbinguni. Basi Tutakuelekeza Qiblah unachokiridhia.” (02:144)
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Ahmad al-Qurtwubiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Qam´-ul-Hirsw biz-Zuhd wal-Qanaa´ah, uk. 45
- Imechapishwa: 18/03/2017
47- Ni katika adabu mtu kuashiria haja yake. Hivyo ndivyo walivyokuwa wakifanya Mitume na watu bora na mawalii waliowafuata.
48- Allaah (Ta´ala) amesema:
وَأَيُّوبَ إِذْ نَادَىٰ رَبَّهُ أَنِّي مَسَّنِيَ الضُّرُّ وَأَنتَ أَرْحَمُ الرَّاحِمِينَ
“Na Ayyuub alipomwita Mola wake [akiomba]: “Hakika mimi imenigusa dhara, Nawe ndiye mbora zaidi wa kurehemu kuliko wengine wote wenye kurehemu”. (21:83)
Aliashiria tu na hakuomba moja kwa moja. Hali kadhalika ndivyo alivyofanya Muusa wakati alipokuwa amekaa chini ya kivuli:
فَسَقَىٰ لَهُمَا ثُمَّ تَوَلَّىٰ إِلَى الظِّلِّ فَقَالَ رَبِّ إِنِّي لِمَا أَنزَلْتَ إِلَيَّ مِنْ خَيْرٍ فَقِيرٌ
“Basi akawanyweshea, kisha akageuka kwenda kivulini, akasema: “Mola wangu! Hakika mimi ni mhitajia wa kheri Utakayoniteremshia.” (28:24)
Alikuwa ni mwenye njaa alipoashiria hivyo. Na Mtume wetu (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akiangalia mbinguni akiashiria maombi. Hapo ndipo akaambiwa:
قَدْ نَرَىٰ تَقَلُّبَ وَجْهِكَ فِي السَّمَاءِ ۖ فَلَنُوَلِّيَنَّكَ قِبْلَةً تَرْضَاهَا
“Hakika Tumeona unavyogeuzageuza uso wako mbinguni. Basi Tutakuelekeza Qiblah unachokiridhia.” (02:144)
Mhusika: Imaam Muhammad bin Ahmad al-Qurtwubiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Qam´-ul-Hirsw biz-Zuhd wal-Qanaa´ah, uk. 45
Imechapishwa: 18/03/2017
https://firqatunnajia.com/15881-2/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)