Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akakaa baadhi ya siku Qubaa´. Maoni mengine yanasema kuwa alikaa siku kumi na nne. Huko ndio akaasisi msingi wa Qubaa´. Baada ya hapo akaendelea na safari yake kwa maamrisho ya Allaah (Ta´ala). Ilikuwa ni siku ya Ijumaa ndio alifika kwa Banuu Saalim bin ´Awf. Akaswali swalah ya Ijumaa kwenye msikiti wa Raanuunaa bondeni. Watu wa kabila wakamuomba (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aishi kati yao, akasema:
“Iacheni ngamia. Hakika ni yenye kuamrishwa.”[1]
Wakati ilipofika mahali ambapo msikiti wake upo hii leo, ikapiga magoti. Hakuteremka (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) mpaka pale ilipoinuka tena, ikapiga tambo kidogo, ikageuka kisha ikapiga magoti ile sehemu ya kwanza ilipoanda kupiga magoti. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akashuka. Ilikuwa kwa Banuun-Najjaar. Abu Ayyuub akabeba mabegi ya Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) nyumbani kwake. Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akanunua ardhi ya msikiti. Hapo kabla ilikuwa ni mahali pa mayatima wawili wanapofugia ngamia. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akafanya sehemu hiyo kuwa msikiti na ndio msikiti wake hii leo. Karibu yake akajenga nyumba ya wake zake.
Kuhusiana na ´Aliy (Radhiya Allaahu ´anh) alibaki Makkah ili kurudisha nafasi za watu walizokuwa nazo kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na mambo mengine. Kisha baada ya hapo na yeye akajiunga na Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
[1] al-Bayhaqiy katika ”Dalaa-il-un-Nubuwwah” (2/508). Dhaifu kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”adh-Dhwa´iyfah” (6508).
- Mhusika: Imaam Ismaa´iyl bin Kathiyr ad-Dimashqiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Fusuwl fiy Siyrat-ir-Rasuwl, uk. 38-39
- Imechapishwa: 18/03/2017
Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akakaa baadhi ya siku Qubaa´. Maoni mengine yanasema kuwa alikaa siku kumi na nne. Huko ndio akaasisi msingi wa Qubaa´. Baada ya hapo akaendelea na safari yake kwa maamrisho ya Allaah (Ta´ala). Ilikuwa ni siku ya Ijumaa ndio alifika kwa Banuu Saalim bin ´Awf. Akaswali swalah ya Ijumaa kwenye msikiti wa Raanuunaa bondeni. Watu wa kabila wakamuomba (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aishi kati yao, akasema:
“Iacheni ngamia. Hakika ni yenye kuamrishwa.”[1]
Wakati ilipofika mahali ambapo msikiti wake upo hii leo, ikapiga magoti. Hakuteremka (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) mpaka pale ilipoinuka tena, ikapiga tambo kidogo, ikageuka kisha ikapiga magoti ile sehemu ya kwanza ilipoanda kupiga magoti. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akashuka. Ilikuwa kwa Banuun-Najjaar. Abu Ayyuub akabeba mabegi ya Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) nyumbani kwake. Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akanunua ardhi ya msikiti. Hapo kabla ilikuwa ni mahali pa mayatima wawili wanapofugia ngamia. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akafanya sehemu hiyo kuwa msikiti na ndio msikiti wake hii leo. Karibu yake akajenga nyumba ya wake zake.
Kuhusiana na ´Aliy (Radhiya Allaahu ´anh) alibaki Makkah ili kurudisha nafasi za watu walizokuwa nazo kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na mambo mengine. Kisha baada ya hapo na yeye akajiunga na Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
[1] al-Bayhaqiy katika ”Dalaa-il-un-Nubuwwah” (2/508). Dhaifu kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”adh-Dhwa´iyfah” (6508).
Mhusika: Imaam Ismaa´iyl bin Kathiyr ad-Dimashqiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Fusuwl fiy Siyrat-ir-Rasuwl, uk. 38-39
Imechapishwa: 18/03/2017
https://firqatunnajia.com/15-kukaa-al-madiynah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)