Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amekokoteza juu ya kujifunza elimu yenye manufaa na kuifanyia kazi. Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) amesema:
وَمَا كَانَ الْمُؤْمِنُونَ لِيَنفِرُوا كَافَّةً ۚ فَلَوْلَا نَفَرَ مِن كُلِّ فِرْقَةٍ مِّنْهُمْ طَائِفَةٌ لِّيَتَفَقَّهُوا فِي الدِّينِ وَلِيُنذِرُوا قَوْمَهُمْ إِذَا رَجَعُوا إِلَيْهِمْ لَعَلَّهُمْ يَحْذَرُونَ
”Haiwapasi waumini watoke wote pamoja kwenda [vitani]. Hivyo basi kwanini lisitoke katika kila kundi miongoni mwao kundi moja wajifunze dini na ili wawaonye watu wao watakaporejea kwao ili wapate kujitahadharisha.” (at-Tawbah 09:122)
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Yule ambaye Allaah anamtakia kheri, basi humpa ufahamu akaifahamu dini.”[1]
Kuwa na ufahamu katika dini na kujifunza elimu yenye manufaa ni katika alama zinazoonyesha kuwa Allaah anamtakia kheri mtu. Sambamba na hilo kupuuza kujifunza dini ni katika zinazoonyesha kuwa Allaah anamtakia shari mtu.
[1] Ameipokea al-Bukhaariy (71) na Muslim (1037).
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Nawaaqidh-il-Islaam, uk. 189
- Imechapishwa: 13/03/2019
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amekokoteza juu ya kujifunza elimu yenye manufaa na kuifanyia kazi. Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) amesema:
وَمَا كَانَ الْمُؤْمِنُونَ لِيَنفِرُوا كَافَّةً ۚ فَلَوْلَا نَفَرَ مِن كُلِّ فِرْقَةٍ مِّنْهُمْ طَائِفَةٌ لِّيَتَفَقَّهُوا فِي الدِّينِ وَلِيُنذِرُوا قَوْمَهُمْ إِذَا رَجَعُوا إِلَيْهِمْ لَعَلَّهُمْ يَحْذَرُونَ
”Haiwapasi waumini watoke wote pamoja kwenda [vitani]. Hivyo basi kwanini lisitoke katika kila kundi miongoni mwao kundi moja wajifunze dini na ili wawaonye watu wao watakaporejea kwao ili wapate kujitahadharisha.” (at-Tawbah 09:122)
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Yule ambaye Allaah anamtakia kheri, basi humpa ufahamu akaifahamu dini.”[1]
Kuwa na ufahamu katika dini na kujifunza elimu yenye manufaa ni katika alama zinazoonyesha kuwa Allaah anamtakia kheri mtu. Sambamba na hilo kupuuza kujifunza dini ni katika zinazoonyesha kuwa Allaah anamtakia shari mtu.
[1] Ameipokea al-Bukhaariy (71) na Muslim (1037).
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Nawaaqidh-il-Islaam, uk. 189
Imechapishwa: 13/03/2019
https://firqatunnajia.com/148-mahimizo-ya-allaah-na-mtume-wake-kujifunza-dini/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)