2- Daku imependekezwa. Allaah (Ta´ala) amesema:
وَكُلُوا وَاشْرَبُوا حَتَّىٰ يَتَبَيَّنَ لَكُمُ الْخَيْطُ الْأَبْيَضُ مِنَ الْخَيْطِ الْأَسْوَدِ مِنَ الْفَجْرِ
“Kuleni na kunyweni mpaka ubainike kwenu uzi mweupe wa alfajiri kutokana na uzi mweusi.”[1]
al-Bukhaariy na Muslim wamepokea kupitia kwa ´Umar (Radhiya Allaahu ´anh) ambaye ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa na waadhini wawili; Bilaal na Ibn Umm Maktuum ambaye alikuwa kipofu ambapo Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema:
“Bilaal anaadhini usiku. Hivyo kuleni na kunyweni mpaka aadhini Ibn Umm Maktuum.”
Qaasim bin Muhammad – ambaye ni mmoja wa wapokezi wa Hadiyth hiyo – amesema:
“Hakukuwa na kitambo kirefu baina ya muadhini wa kwanza na wa pili.”[2]
Miongoni mwa dalili za kwamba daku imependekezwa ni yale yaliyothibiti kwa al-Bukhaariy na Muslim kupitia kwa Anas (Radhiya Allaahu ´anh) ambaye ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Kuleni daku. Kwani katika daku kuna baraka.”[3]
3- Imependekezwa kuichelewesha daku. Hayo ni kutokana na yale yaliyopokelewa katika “as-Swahiyh” ya Muslim kupitia kwa ´Amr bin al-´Aasw (Radhiya Allaahu ´anh) aliyesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Kipambanuzi kati ya swawm yetu na swawm ya Ahl-ul-Kitaab ni kula daku.”[4]
[1] 02:187
[2] al-Bukhaariy (617) na Muslim (1092).
[3] al-Bukhaariy (1923) na Muslim (1095).
[4] Muslim (1096).
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Mukhtaswaru fiy Ahkaam-is-Swiyaam, uk. 19-21
- Imechapishwa: 23/05/2019
2- Daku imependekezwa. Allaah (Ta´ala) amesema:
وَكُلُوا وَاشْرَبُوا حَتَّىٰ يَتَبَيَّنَ لَكُمُ الْخَيْطُ الْأَبْيَضُ مِنَ الْخَيْطِ الْأَسْوَدِ مِنَ الْفَجْرِ
“Kuleni na kunyweni mpaka ubainike kwenu uzi mweupe wa alfajiri kutokana na uzi mweusi.”[1]
al-Bukhaariy na Muslim wamepokea kupitia kwa ´Umar (Radhiya Allaahu ´anh) ambaye ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa na waadhini wawili; Bilaal na Ibn Umm Maktuum ambaye alikuwa kipofu ambapo Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema:
“Bilaal anaadhini usiku. Hivyo kuleni na kunyweni mpaka aadhini Ibn Umm Maktuum.”
Qaasim bin Muhammad – ambaye ni mmoja wa wapokezi wa Hadiyth hiyo – amesema:
“Hakukuwa na kitambo kirefu baina ya muadhini wa kwanza na wa pili.”[2]
Miongoni mwa dalili za kwamba daku imependekezwa ni yale yaliyothibiti kwa al-Bukhaariy na Muslim kupitia kwa Anas (Radhiya Allaahu ´anh) ambaye ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Kuleni daku. Kwani katika daku kuna baraka.”[3]
3- Imependekezwa kuichelewesha daku. Hayo ni kutokana na yale yaliyopokelewa katika “as-Swahiyh” ya Muslim kupitia kwa ´Amr bin al-´Aasw (Radhiya Allaahu ´anh) aliyesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Kipambanuzi kati ya swawm yetu na swawm ya Ahl-ul-Kitaab ni kula daku.”[4]
[1] 02:187
[2] al-Bukhaariy (617) na Muslim (1092).
[3] al-Bukhaariy (1923) na Muslim (1095).
[4] Muslim (1096).
Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Mukhtaswaru fiy Ahkaam-is-Swiyaam, uk. 19-21
Imechapishwa: 23/05/2019
https://firqatunnajia.com/14-mapendekezo-ya-daku-na-kuichelewesha/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)