Shaykh Bakr amesema:

“Kitu cha kwanza nilichofanya nilikimbia huko na kuona kuwa inahusiana na nukuu moja katika misitari kadhaa kutoka katika kitabu chake “al-´Adaalah al-Ijtimaa´iyyah”. Niliona kuwa maneno yake hayaafikiani na kichwa cha khabari hichi cha uchokozi. Wacha tuseme kuwa maneno yake kweli yana ibara zisizokuwa wazi na zisizofungamana. Ni vipi mtu anaweza kuyafanya yakawa ni makosa ya kikafiri na kubomoa yote ambayo Sayyid Qutwub (Rahimahu Allaah) amejenga maisha yake juu yake kwa vile alilingania katika Tawhiyd ya Allaah katika hukumu na uwekaji wa Shari´ah na akatupilia mbali sheria za wanaadamu zilizotungwa na akakabiliana na wale wenye kuhukumu kwazo? Hakika Allaah anapenda uadilifu na inswafu katika kila kitu. Sikuonelei isipokuwa – Allaah akitaka – utarejea katika uadilifu na inswafu.”

Shaykh Bakr anatumbukia katika makosa mengi ambayo baadhi ni kutonukuu yale anayonikosoa kwayo. Uhakika wa mambo kamwe hafanyi hivo. Kama tulivyosema anatumbukia katika makosa mengi. Baadhi yake ni kuwa Shaykh Bakr hanukuu yale niliyonukuu katika maneno ya Sayyid katika “al-´Adaalah al-Ijtimaa´iyyah”. Humo Sayyid amesema wazi kabisa kwamba inajuzu uwekaji wa Shari´ah na kwamba mtu anaweza kustafidi sheria za wanaadamu zote midhali hazikhalifu misingi ya Uislamu. Kwa msemo mwingine anakusudia utungaji kanuni wa ulaya, marekani na urusi. Ni vipi misingi ya ukafiri na ukanamungu itaafikiana na misingi ya Uislamu? Malengo ya Sayyid ni pamoja vilevile na uongozi wa ujamaa na pia kutokomeza utumwa. Ni maneno ya wazi juu ya kujuzu kwa kanuni za wanaadamu. Kwa hiyo Shaykh Bakr anaacha kuyanukuu maneno yake ili kumghuri msomaji.

Kadhalika Shaykh Bakr anasema:

“Wacha tuseme kuwa maneno yake kweli yana ibara zisizokuwa wazi na zisizofungamana. Ni vipi mtu anaweza kuyafanya yakawa ni makosa ya kikafiri… “

Huu ndio uchokozi wa batili. Katika ya batili ni maneno yake Shaykh Bakr kwamba chini ya kichwa cha khabari nina nukuu moja tu. Si kweli kabisa. Nilimraddi Sayyid sehemu nyingi ili kuonyesha ubaya wa namna anavyoweka kanuni na kwamba kitendo cha uwekaji sheria ni batili.