1- Imependekezwa kuharakisha kukata swawm pale kunapohakikishwa kwa macho kuwa jua limezama au mtu akaelezwa na mtu mwaminifu na mwadilifu. Hayo ni kutokana na yale yaliyothibiti kwa al-Bukhaariy na Muslim kupitia kwa Sahl bin Sa´d (Radhiya Allaahu ´anh) aliyeeleza kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Wato hawatoacha kuwa katika kheri muda ya kuwa wanaharakisha kukata swawm.”
Hayo ni kwa sababu kuharakisha kukata swawm kunafahamisha utekelezaji [wa maamrisho ya Allaah] na kuchelewesha kunafahamisha kuchupa mipaka. Hayo yanafanywa na mayahudi na manaswara na baadhi ya mapote yaliyopinda ambayo yanachelewesha kukata swawm mpaka kunachomoza nyota. Katika “as-Sunan” ya Abu Daawuud imepokelewa:
“Mayahudi na manaswara ndio wenye kuchelewesha.”
Ibn Hibbaan na al-Haakim wamepokea kupitia kwa Sahl (Radhiya Allaahu ´anh) kwa tamko linalosema:
“Ummah wangu utaendelea kuwa juu ya mwenendo wangu muda wa kuwa wakati wa kukata kwao swawm hawasubiri kuchomoza kwa nyota.”[1]
[1] Ibn Hibbaan (3510) na al-Haakim (1584) ambaye amesema:
”Hadiyth hii iko kwa mujibu wa masharti ya al-Bukhaariy na Muslim na hawakuipokea kwa mtiririko kama huu.”
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Mukhtaswaru fiy Ahkaam-is-Swiyaam, uk. 19
- Imechapishwa: 23/05/2019
1- Imependekezwa kuharakisha kukata swawm pale kunapohakikishwa kwa macho kuwa jua limezama au mtu akaelezwa na mtu mwaminifu na mwadilifu. Hayo ni kutokana na yale yaliyothibiti kwa al-Bukhaariy na Muslim kupitia kwa Sahl bin Sa´d (Radhiya Allaahu ´anh) aliyeeleza kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Wato hawatoacha kuwa katika kheri muda ya kuwa wanaharakisha kukata swawm.”
Hayo ni kwa sababu kuharakisha kukata swawm kunafahamisha utekelezaji [wa maamrisho ya Allaah] na kuchelewesha kunafahamisha kuchupa mipaka. Hayo yanafanywa na mayahudi na manaswara na baadhi ya mapote yaliyopinda ambayo yanachelewesha kukata swawm mpaka kunachomoza nyota. Katika “as-Sunan” ya Abu Daawuud imepokelewa:
“Mayahudi na manaswara ndio wenye kuchelewesha.”
Ibn Hibbaan na al-Haakim wamepokea kupitia kwa Sahl (Radhiya Allaahu ´anh) kwa tamko linalosema:
“Ummah wangu utaendelea kuwa juu ya mwenendo wangu muda wa kuwa wakati wa kukata kwao swawm hawasubiri kuchomoza kwa nyota.”[1]
[1] Ibn Hibbaan (3510) na al-Haakim (1584) ambaye amesema:
”Hadiyth hii iko kwa mujibu wa masharti ya al-Bukhaariy na Muslim na hawakuipokea kwa mtiririko kama huu.”
Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Mukhtaswaru fiy Ahkaam-is-Swiyaam, uk. 19
Imechapishwa: 23/05/2019
https://firqatunnajia.com/13-mapendekezo-ya-kuharikisha-kukata-swawm-futari/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)