Daraja ya tatu: Utashi. Allaah (Tabaarak wa Ta´ala) amekitaka kila kilichopo au kisichokuwepo mbinguni au ardhini. Kilichopo kipo kwa kuwa Allaah (Ta´ala) ametaka kiwepo. Kisichokuwepo hakipo kwa kuwa Allaah (Ta´ala) ametaka kisiwepo. Haya yako dhahiri katika Qur-aan tukufu. Allaah (Ta´ala) amethibitisha matakwa Yake katika matendo Yake na katika matendo ya waja. Allaah (Ta´ala) amesema:
إِنْ هُوَ إِلَّا ذِكْرٌ لِّلْعَالَمِينَ لِمَن شَاءَ مِنكُمْ أَن يَسْتَقِيمَ وَمَا تَشَاءُونَ إِلَّا أَن يَشَاءَ اللَّـهُ رَبُّ الْعَالَمِينَ
“Hichi [Kitabu] si jengine isipokuwa ni ukumbusho kwa walimwengu – kwa yule anayetaka miongoni mwenu anyooke. Lakini hamtotaka isipokuwa atake Allaah, Mola wa walimwengu.”[1]
وَلَوْ شَاءَ رَبُّكَ مَا فَعَلُوهُ
“Na lau Angetaka Mola wako wasingeliyafanya hayo.”[2]
وَلَوْ شَاءَ اللَّـهُ مَا اقْتَتَلَ الَّذِينَ مِن بَعْدِهِم مِّن بَعْدِ مَا جَاءَتْهُمُ الْبَيِّنَاتُ
“Lau angelitaka Allaah wasingelipigana wale wa baada yao baada ya kuwajilia hoja za wazi.”[3]
Allaah (Ta´ala) amebainisha kuwa matendo ya waja yanapitika kwa matakwa Yake.
Kuhusu matendo Yake (Ta´ala), mara nyingi yametajwa:
وَلَوْ شِئْنَا لَآتَيْنَا كُلَّ نَفْسٍ هُدَاهَا
“Tungelitaka, Tungeliipa kila nafsi mwongozo wake.”[4]
وَلَوْ شَاءَ رَبُّكَ لَجَعَلَ النَّاسَ أُمَّةً وَاحِدَةً
“Kama angetaka Mola wako bila shaka Angewafanya watu wote kuwa ni ummah mmoja.”[5]
Kuna Aayah nyingi zinazothibitisha matakwa katika matendo ya Allaah (Tabaarak wa Ta´ala).
Imani ya kuamini makadirio haitimii isipokuwa mpaka tuamini kuwa kila kilichopo na kisichokuwepo kinatokamana na matakwa ya Allaah. Hakuna kisichokuwepo isipokuwa Allaah (Ta´ala) ametaka kisiwepo. Na hakuna kilichopo isipokuwa Allaah (Ta´ala) ametaka kiwepo. Haiwezekani kukawepo kitu mbinguni wala ardhini isipokuwa kwa utashi wa Allaah (Ta´ala).
[1] 81:27-29
[2] 06:112
[3] 02:253
[4] 32:13
[5] 11:118
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Qadhwaa’ wal-Qadar, katika Majmuu´-ul-Fataawaa (5/224-225)
- Imechapishwa: 25/10/2016
Daraja ya tatu: Utashi. Allaah (Tabaarak wa Ta´ala) amekitaka kila kilichopo au kisichokuwepo mbinguni au ardhini. Kilichopo kipo kwa kuwa Allaah (Ta´ala) ametaka kiwepo. Kisichokuwepo hakipo kwa kuwa Allaah (Ta´ala) ametaka kisiwepo. Haya yako dhahiri katika Qur-aan tukufu. Allaah (Ta´ala) amethibitisha matakwa Yake katika matendo Yake na katika matendo ya waja. Allaah (Ta´ala) amesema:
إِنْ هُوَ إِلَّا ذِكْرٌ لِّلْعَالَمِينَ لِمَن شَاءَ مِنكُمْ أَن يَسْتَقِيمَ وَمَا تَشَاءُونَ إِلَّا أَن يَشَاءَ اللَّـهُ رَبُّ الْعَالَمِينَ
“Hichi [Kitabu] si jengine isipokuwa ni ukumbusho kwa walimwengu – kwa yule anayetaka miongoni mwenu anyooke. Lakini hamtotaka isipokuwa atake Allaah, Mola wa walimwengu.”[1]
وَلَوْ شَاءَ رَبُّكَ مَا فَعَلُوهُ
“Na lau Angetaka Mola wako wasingeliyafanya hayo.”[2]
وَلَوْ شَاءَ اللَّـهُ مَا اقْتَتَلَ الَّذِينَ مِن بَعْدِهِم مِّن بَعْدِ مَا جَاءَتْهُمُ الْبَيِّنَاتُ
“Lau angelitaka Allaah wasingelipigana wale wa baada yao baada ya kuwajilia hoja za wazi.”[3]
Allaah (Ta´ala) amebainisha kuwa matendo ya waja yanapitika kwa matakwa Yake.
Kuhusu matendo Yake (Ta´ala), mara nyingi yametajwa:
وَلَوْ شِئْنَا لَآتَيْنَا كُلَّ نَفْسٍ هُدَاهَا
“Tungelitaka, Tungeliipa kila nafsi mwongozo wake.”[4]
وَلَوْ شَاءَ رَبُّكَ لَجَعَلَ النَّاسَ أُمَّةً وَاحِدَةً
“Kama angetaka Mola wako bila shaka Angewafanya watu wote kuwa ni ummah mmoja.”[5]
Kuna Aayah nyingi zinazothibitisha matakwa katika matendo ya Allaah (Tabaarak wa Ta´ala).
Imani ya kuamini makadirio haitimii isipokuwa mpaka tuamini kuwa kila kilichopo na kisichokuwepo kinatokamana na matakwa ya Allaah. Hakuna kisichokuwepo isipokuwa Allaah (Ta´ala) ametaka kisiwepo. Na hakuna kilichopo isipokuwa Allaah (Ta´ala) ametaka kiwepo. Haiwezekani kukawepo kitu mbinguni wala ardhini isipokuwa kwa utashi wa Allaah (Ta´ala).
[1] 81:27-29
[2] 06:112
[3] 02:253
[4] 32:13
[5] 11:118
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Qadhwaa’ wal-Qadar, katika Majmuu´-ul-Fataawaa (5/224-225)
Imechapishwa: 25/10/2016
https://firqatunnajia.com/13-daraja-ya-tatu-ya-makadirio-matakwa/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)