128. al-Qummiy upotoshaji wake wa nane wa al-An´aam

al-Qummiy amesema wakati alipokuwa akifasiri Aayah:

إِنَّ اللَّـهَ فَالِقُ الْحَبِّ وَالنَّوَىٰ

“Hakika Allaah ndiye hufanya mbegu na kokwa zikapasuka.”[1]

“Mbegu ni yale yanayopendwa na kokwa ni kupinda kutoka katika haki.”

Amesema vilevile:

“Mbegu ni elimu kuzimwa kutoka kwa maimamu na kokwa ni yale yote yenye kujitenga mbali nayo.”

al-Qummiy amesema kuhusu:

وَهُوَ الَّذِي جَعَلَ لَكُمُ النُّجُومَ لِتَهْتَدُوا بِهَا فِي ظُلُمَاتِ الْبَرِّ وَالْبَحْرِ

“Yeye ndiye ambaye Aliyekufanyieni nyota ili muongozwe kwazo katika viza vya nchikavu na bahari.”[2]

“Nyota ni kizazi cha Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).”[3]

Allaah ametakasika kutokamana na yale wanayosema madhalimu Baatwiniyyah. Kitabu cha Allaah kiko wazi na ujumbe Wake uko wazi vilevile na unawazungumzisha watu wote. Hawazungumzishi Baatwiniyyah kwa njia zao, alama zao na nembo zao. Si jengine isipokuwa ni ujumbe ulio wazi kabisa.

Kila mmoja anajua ni nini mbegu na kokwa. Kila mmoja anajua nini maana ya nyota. Ni miongoni mwa neema za Allaah juu ya waja Wake, waumini na makafiri. Waumini wanamshukuru kwa neema hizi na Allaah anawakumbusha makafiri neema hizi heunda wakamshukuru na wakarudi katika dini Yake.

[1] 06:95

[2] 06:97

[3] Tafsiyr al-Qummiy (1/211).

  • Mhusika: ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Intiswaar li Kitaab-il-´Aziyz al-Jabbaar, uk. 186
  • Imechapishwa: 17/06/2018