127. Je, inafaa kuvunja mfupa wa maiti kafiri?

Swali 127: Je, inafaa kuvunja mfupa wa maiti kafiri[1]?

Jibu: Ni jambo linahitaji upambanuzi. Akiwa ni Dhimmiy au ambaye amepewa mkataba wa amani au amepewa ulinzi haijuzu kumshambulia. Lakini hapana neno akiwa ni kafiri wa vita. Kujengea juu ya hayo inafaa kuchukua viungo vya waliokufa katika makafiri wa vita. Kuhusu Dhimmiy, ambaye amepewa mkataba wa amani au amepewa ulinzi hapana. Kwa sababu miili yao ni yenye kuheshimiwa.

[1] Majmuu´-ul-Fataawaa (13/363).

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Ahkaam-ul-Janaa-iz, uk. 93
  • Imechapishwa: 15/01/2022