125. al-´Ayyaashiy upotoshaji wake wa tatu wa al-An´aam

al-´Ayyaashiy amesema:

“Muhammad bin Himraan amesema: “Nilikuwa kwa Abu ´Abdillaah ambapo alikuja mtu na kusema: “Ee Abu ´Abdillaah! Si ajabu kwamba ´Iysaa bin Zayd bin ´Aliy anasema kuwa hasimami upande wa ´Aliy isipokuwa tu kidhahiri… [1]“ Akasema: “Sasa nifanye nini? Allaah amesema:

فَإِن يَكْفُرْ بِهَا هَـٰؤُلَاءِ فَقَدْ وَكَّلْنَا بِهَا قَوْمًا لَّيْسُوا بِهَا بِكَافِرِينَ

“Wakiyakanusha hawa, basi hakika Tumekwishayawakilisha kwa watu wasioyakanusha.”[2]

Bi maana Maswahabah wake, Quraysh na wale wegine wote wenye kukataa haki ya kula kiapo kwa kiongozi wa waumini:

Akaashiria kwa mkono kwetu sisi. Nikasema: “Naapa kwa Allaah, naelewa.”[3]

Mhakiki amesema:

“Amepokea “al-Burhaan” na “al-Bihaar”. al-Majlisiy amesema wakati alipokuwa akifasiri haya: “Amefasiri watu (قَوْمًا) katika Aayah kama Shiy´ah, kizazi kisichokuwa cha kiarabu… ´Iysaa bin Zayd bin ´Aliy alikuwa ´Iysaa bin Zayd bin ´Aliy bin al-Husayn bin ´Aliy. Shaykh amemzingatia kuwa katika watu wa as-Swaadiq. Kwa udhahiri ni kwamba alikuwa Imaamiy, lakini hata hivyo alikuwa mbaya, kama yanavyofahamisha mapokezi yake mengi… “

Allaah amemtakaa Abu ´Abdillaah kutokamana na uongo huu. Malengo ya maneno haya yaliyozuliwa ni kwamba anathibitisha uongozi na anamkufurisha yule ambaye hauamini kwa udhahiri na kwa ndani.

Tazama namna ambavyo al-Majlisiy anavofasiri watu katika Aayah kwamba ni Shiy´ah, kizazi kisichokuwa cha kiarabu, wafursi. Kwa msemo mwingine ni kwamba Maswahabah walikufuru na Shiy´ah, kizazi kisichokuwa cha kiarabu na wafursi, ndio waliowakilishwa na Allaah. Lakini hata hivyo sisi tunasema kuwa Maswahabah ndio waliowakilishwa kwa Kitabu, hukumu na utume. Ama kuhusu Shiy´ah wafursi Raafidhwah, hakuna jengine walichofanya isipokuwa tu ni kuamini uongozi waliozuliwa na Ibn Sabaa´. Tofauti hii inatosha kati ya makundi hayo mawili.

[1] Hapa kumetajwa maneno ya khatari ambayo kwa kweli sikuweza kuyataja, khaswa kwa kuzingatia ya kwamba ni ya uongo dhidi ya ´Iysaa bin Zayd bin ´Aliy.

[2] 06:89

[3] Tafsiyr al-´Ayyaashiy (1/367-368).

  • Mhusika: ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Intiswaar li Kitaab-il-´Aziyz al-Jabbaar, uk. 183
  • Imechapishwa: 17/06/2018