124. al-Qummiy upotoshaji wake wa sita wa al-An´aam

al-Qummiy amesema pindi alipokuwa akifasiri maneno ya Allaah (Ta´ala):

وَوَهَبْنَا لَهُ إِسْحَاقَ وَيَعْقُوبَ ۚ كُلًّا هَدَيْنَا ۚ وَنُوحًا هَدَيْنَا مِن قَبْلُ ۖ وَمِن ذُرِّيَّتِهِ دَاوُودَ وَسُلَيْمَانَ وَأَيُّوبَ وَيُوسُفَ وَمُوسَىٰ وَهَارُونَ ۚ وَكَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ وَزَكَرِيَّا وَيَحْيَىٰ وَعِيسَىٰ وَإِلْيَاسَ ۖ كُلٌّ مِّنَ الصَّالِحِينَ وَإِسْمَاعِيلَ وَالْيَسَعَ وَيُونُسَ وَلُوطًا ۚ وَكُلًّا فَضَّلْنَا عَلَى الْعَالَمِينَ وَمِنْ آبَائِهِمْ وَذُرِّيَّاتِهِمْ وَإِخْوَانِهِمْ ۖ وَاجْتَبَيْنَاهُمْ وَهَدَيْنَاهُمْ إِلَىٰ صِرَاطٍ مُّسْتَقِيمٍ ذَٰلِكَ هُدَى اللَّـهِ يَهْدِي بِهِ مَن يَشَاءُ مِنْ عِبَادِهِ ۚ وَلَوْ أَشْرَكُوا لَحَبِطَ عَنْهُم مَّا كَانُوا يَعْمَلُونَ  أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ آتَيْنَاهُمُ الْكِتَابَ وَالْحُكْمَ وَالنُّبُوَّةَ

“Tukamtunukia Ishaaq na Ya’quub, wote Tukawaongoza [kama ambavo] Nuuh tulimwongoza hapo kabla. Na katika kizazi chake Daawuud na Sulaymaan na Ayyuub na Yuusuf na Muusa na Haaruun – na hivyo ndivo Tulipavyo wafanyao wema – na Zakariyyaa na Yahyaa na ‘Iysaa na Ilyaas – wote ni miongoni mwa waja wema – na Ismaa’iyl na Ilyasaa´ na Yuunus na Luutw – na wote Tuliwafadhilisha juu ya walimwengu – na katika baba zao na kizazi chao na ndugu zao. Tukawateua na tukawaongoza katika njia iliyonyooka. Huo ndio mwongozo wa Allaah [ambao]  humwongoza amtakaye kati ya waja Wake. Lau wangemshirikisha bila shaka yangeharibika yale yote waliyokuwa wakifanya. Hao ndio wale Tuliowapa Kitabu na hekima na utume.”[1]

“Bi maana hao Mitume ambao wametangulia kutajwa. Kisha akasema:

فَإِن يَكْفُرْ بِهَا هَـٰؤُلَاءِ

“Wakiyakanusha hawa… “

Bi maana Maswahabah wake, Quraysh na wale wegine wote wenye kukataa haki ya kula kiapo kwa kiongozi wa waumini:

فَقَدْ وَكَّلْنَا بِهَا قَوْمًا لَّيْسُوا بِهَا بِكَافِرِينَ

“… basi hakika Tumekwishayawakilisha kwa watu wasioyakanusha.”[2]

Bi maana kundi la kiongozi wa waumini.”[3]

Hakuinasibisha tafsiri hii kwa yeyote katika watu wa nyumbani kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kama ilivyo kawaida yake.

Haafidhwh Ibn Kathiyr amesema katika tafsiri yake ya Qur-aan:

وَلَوْ أَشْرَكُوا لَحَبِطَ عَنْهُم مَّا كَانُوا يَعْمَلُونَ

“Lau wangemshirikisha bila shaka yangeharibika yale yote waliyokuwa wakifanya.”

kunaonysha ni ukali na ukhatari ulivyo wa jambo la shirki. Ni kama mfano wa maneno Yake (Ta´ala):

وَلَقَدْ أُوحِيَ إِلَيْكَ وَإِلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكَ لَئِنْ أَشْرَكْتَ لَيَحْبَطَنَّ عَمَلُكَ وَلَتَكُونَنَّ مِنَ الْخَاسِرِينَ

“Hakika umefunuliwa Wahy na kwa wale walio kabla yako kwamba: “Ukifanya shirki, bila shaka yataharibika matendo yako na utakuwa miongoni mwa waliokhasirika.”[4]

Hii ni sharti na sharti haipelekei ule uhalisia wa mambo utokee. Ni kama mfano wa maneno Yake Allaah (Ta´ala):

قُلْ إِن كَانَ لِلرَّحْمَـٰنِ وَلَدٌ فَأَنَا أَوَّلُ الْعَابِدِينَ

“Sema: “Kama ingelikuwa Mwingi wa huruma ana mwana, basi mimi ningekuwa wa mwanzo kumwabudu.”[5]

Zingatia tafsiri ya al-Qummiy juu ya maneno ya Allaah (Ta´ala):

فَإِن يَكْفُرْ بِهَا هَـٰؤُلَاءِ

“Wakiyakanusha hawa… “

Bi maana Maswahabah wake, Quraysh na wale wegine wote wenye kukataa haki ya kula kiapo kwa kiongozi wa waumini.”

Allaah akuue! Ni ujasiri ulioje ulionao wa kukipotosha Kitabu cha Allaah na kuwakufurisha Maswahabah wa Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambao ni watu wakweli na wenye Ikhlaasw amabo hawajapatapo kuonekana baada ya Manabii na Mitume! Hakuna ambaye ni mbora wala mkamilifu zaidi kuliko wao. Hakuna yeyote aliyeinusuru dini ya Allaah kwa nguvu kama walivofanya wao. Ee Baatwiniy! Hapa kiapo cha utiifu kinahusiana na nini? Ni wakati gani Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliamrisha kiapo hiki? Hakika dhamiri katika Aayah:

فَإِن يَكْفُرْبِهَاهَؤُلاء

“Wakiyakanusha hawa… “

inarudi katika uteremsho, hekima na utume. Hicho kiapo kimeingia vipi? Aayah hii inawalenga makafiri wa Quraysh na wale wakaidi waliopingana na Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), na sio Maswahabah wa Muhammad  (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Maneno Yake (Ta´ala):

فَقَدْ وَكَّلْنَا بِهَا قَوْمًا لَّيْسُوا بِهَا بِكَافِرِينَ

“… basi hakika Tumekwishayawakilisha kwa watu wasioyakanusha.”

ni Maswahabah wa Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika Muhaajiruun na Answaar na wale wafuasi wao hadi siku ya Qiyaamah. Hawakupinga chochote katika hayo na wala hawakurudisha  herufi hata moja. Waliiamini Qur-aan yote, zile Aayah zilizo wazi na zile zisizokuwa wazi. Hivi ndivyo alivosema Haafidhw Ibn Kathiyr katika tafsiri ya Qur-aan yake[6], jambo ambalo ndilo la haki linaloaminiwa na waumini wote. Hakuna wengine wanaopinga isipokuwa tu Raafidhwah Baatwiniyyah.

Baatwiniy huyu amesema alipokuwa akifasiri maneno Yake Allaah (Ta´ala):

فَقَدْ وَكَّلْنَا بِهَا قَوْمًا لَّيْسُوا بِهَا بِكَافِرِينَ

“… basi hakika Tumekwishayawakilisha kwa watu wasioyakanusha.”

“Bi maana kundi la kiongozi wa waumini.”

Tazama namna ambavo anawakufurisha Maswahabah wa Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), kuwaondoa katika ngazi yao waliowekwa na Allaah na badala yake eti anawaweka wale wanaoitwa kundi la kiongozi wa waumini. Allaah amemtakasa kiongozi wa waumini kutokamana  na Raafidhwah Baatwiniyyah hawa ambao wanajinasibisha kwake kwa dhuluma na uongo kabisa. Wao si wengine isipokuwa ni kundi na jeshi la Shaytwaan.

[1] 06:84-88

[2] 06:89

[3] Tafsiyr al-Qummiy (1/209).

[4] 39:65

[5] 43:81

[6] Tafsiyr-ul-Qur-aan al-´Adhwiym (6/109).

  • Mhusika: ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Intiswaar li Kitaab-il-´Aziyz al-Jabbaar, uk. 183
  • Imechapishwa: 17/06/2018