Shaykh-ul-Islaam na Imaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
Sharti ya tisa ni nia na mahala pale ni moyoni. Kuitamka ni Bid´ah. Dalili ni Hadiyth:
“Matendo huzingatiwa kwa nia. Kila mmoja atalipwa kutokana na kile alichonuia.”[1]
MAELEZO
´Ibaadah zote ni lazima kwa mtu azitilie nia; kama mfano wa swalah, swawm na nyenginezo. ´Ibaadah zote ni lazima kwa mtu azitilie nia. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Matendo huzingatiwa kwa nia. Kila mmoja atalipwa kutokana na kile alichonuia.”
Nia mahala pake ni moyoni. Mahala pa nia katika swalah, swawm na ´ibaadah nyenginezo ni kwenye moyo. Isipokuwa katika hajj. Katika hajj anatakiwa kuisema kwa sauti ule mtindo wa ´ibaadah aliochagua. Hivo ndivo alivofanya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Ama ´ibaadah zengine zote nia iko moyoni.
Kuitamka ni Bid´ah. Kutamka nia kwamba mtu anataka kuswali, anataka kufunga au anataka kutoa swadaqah ni Bid´ah. Isipokuwa tu katika hajj ndio Shari´ah imekuja ikionyesha kudhihirisha Ihraam ya mtu na kusema:
لبيك عمرة
”Nakuitikia ´Umrah.”
لبيك حجا
”Nakuitikia Hajj.”
لبيك عمرة و حجا
”Nakuitikia ´Umrah na Hajj.”
Adhihirishe nia yake iliyomo moyoni. Hii ni Sunnah na kama tulivosema ni jambo maalum katika hajj na ´umrah.
[1] al-Bukhaariy (1) na Muslim (1907).
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: ash-Sharh al-Mumtaaz, uk. 83-84
- Imechapishwa: 30/06/2018
Shaykh-ul-Islaam na Imaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
Sharti ya tisa ni nia na mahala pale ni moyoni. Kuitamka ni Bid´ah. Dalili ni Hadiyth:
“Matendo huzingatiwa kwa nia. Kila mmoja atalipwa kutokana na kile alichonuia.”[1]
MAELEZO
´Ibaadah zote ni lazima kwa mtu azitilie nia; kama mfano wa swalah, swawm na nyenginezo. ´Ibaadah zote ni lazima kwa mtu azitilie nia. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Matendo huzingatiwa kwa nia. Kila mmoja atalipwa kutokana na kile alichonuia.”
Nia mahala pake ni moyoni. Mahala pa nia katika swalah, swawm na ´ibaadah nyenginezo ni kwenye moyo. Isipokuwa katika hajj. Katika hajj anatakiwa kuisema kwa sauti ule mtindo wa ´ibaadah aliochagua. Hivo ndivo alivofanya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Ama ´ibaadah zengine zote nia iko moyoni.
Kuitamka ni Bid´ah. Kutamka nia kwamba mtu anataka kuswali, anataka kufunga au anataka kutoa swadaqah ni Bid´ah. Isipokuwa tu katika hajj ndio Shari´ah imekuja ikionyesha kudhihirisha Ihraam ya mtu na kusema:
لبيك عمرة
”Nakuitikia ´Umrah.”
لبيك حجا
”Nakuitikia Hajj.”
لبيك عمرة و حجا
”Nakuitikia ´Umrah na Hajj.”
Adhihirishe nia yake iliyomo moyoni. Hii ni Sunnah na kama tulivosema ni jambo maalum katika hajj na ´umrah.
[1] al-Bukhaariy (1) na Muslim (1907).
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: ash-Sharh al-Mumtaaz, uk. 83-84
Imechapishwa: 30/06/2018
https://firqatunnajia.com/12-sharti-ya-tisa-ya-swalah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)