12. Hadiyth “Swalah ya ijumaa ilionyeshwa kwa Mtume wa Allaah… “

694- Anas bin Maalik (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:

“Swalah ya ijumaa ilionyeshwa kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Jibriyl (´alayhis-Salaam) ndiye aliyekuja nayo kwake. Ilikuwa kama kio cheupe kilicho na kitu katikati kinachofanana na nukta nyeusi. Akasema: “Ee Jibriyl! Ni kitu gani hichi?” Akasema: “Ni ijumaa. Mola Wako amekuonyesha nayo ili iwe kwako ni sikukuu na kwa watu wako wataokuja baada yako. Ni kheri kwenu. Wewe ndiye utakuwa wa kwanza na mayahudi na manaswara watakuwa baada yako. Ndani yake kuna wakati ambao hakuna yeyote anayemuomba Mola wake juu ya kitu kilicho na kheri ambacho tayari ameshapangiwa isipokuwa humpa kitu hicho, au akaomba ulinzi juu ya kitu kilicho na shari isipokuwa humkinga na kitu kilicho na shari zaidi kuliko hicho.”[1]

Ameipokea at-Twabaraaniy katika “al-Awsatw” kwa mlolongo wa wapokezi mzuri.

[1] Nzuri na Swahiyh. Utimilifu wa Hadiyth utakuja mwishoni mwa kitabu – kwa idhini ya Allaah.

  • Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/435)
  • Imechapishwa: 14/04/2017