´Arshi kilugha ni kiti cha mfalme. Allaah (Ta´ala) amesema kuhusu Yuusuf:
وَرَفَعَ أَبَوَيْهِ عَلَى الْعَرْشِ
“Aliwainua wazazi wake wawili juu ya kiti cha ufalme.”[1]
Vilevile Amesema kuhusu malkia wa Saba´:
وَلَهَا عَرْشٌ عَظِيمٌ
“Na anacho kiti cha ufalme kikubwa.”[2]
Kuhusiana na ´Arshi ya Mwingi wa Rahmah ambayo amelingana juu yake, ni ´Arshi kubwa yenye kuwazunguka viumbe. ´Arshi ndio kiumbe kikubwa kabisa. Abu Dharr (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mbingu saba na ardhi saba ukizilinganisha na Kursiy ni kama mfano wa pete iliyotupwa kwenye jangwa. Na tofauti kati ya ´Arshi na Kursiy ni kama tofauti kati ya jangwa na pete hiyo.”[3]
Mtunzi wa kitabu Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah (Rahimahu Allaah) amesema katika “ar-Risaalah al-´Arshiyyah”:
“Hadiyth hii ina njia nyingi. Imepokelewa na Abu Haatim, Ibn Hibbaan katika “as-Swahiyh”, Ahmad katika “al-Musnad” na wengineo.
Maana ya al-Kursiy kilugha ni kiti ambacho mtu hukaa juu yake. Ama Kursiy ambayo Allaah amejinasibishia nayo ni mahali pa kuwekea miguu Yake miwili (Ta´ala). Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa) amesema:
“Kursiy ni mahala pa kuwekea miguu miwili na ´Arshi hakuna awezaye kuikadiria isipokuwa Allaah (´Azza wa Jall).”[4]
Maana hii iliyotajwa na Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa) ndio yenye kutangaa kwa Ahl-us-Sunnah. Hii ndio sahihi kutoka kwake tofauti na mapokezi yaliyopokelewa yenye kusema kuwa Kursiy maana yake ni elimu. Kadhalika tafsiri ya al-Hasan al-Baswriy yenye kusema kuwa Kursiy maana yake ni ´Arshi ni dhaifu kwa mujibu wa Ibn Kathiyr (Rahimahu Allaah)[5].
[1] 12:100
[2] 27:23
[3] Ibn Hibbaan (94 – al-Mawaarid), Abu Nu´aym katika ”al-Hilyah” (1/167) na al-´Adhwamah (2/569, 649).
[4] al-Haakim amesema:
”Ni Swahiyh juu ya sharti za al-Bukhaariy na Muslim.” (al-Mustadrak (2/282))
adh-Dhahabiy amesema:
”Wapokezi wake ni waaminifu.” (al-´Uluww, uk. 61)
al-Azhariy amesema:
“Wanachuoni wameafikiana juu ya usahihi wa upokezi huu.” (Tahdhib-ul-Lughah (10/61))
[5] Tafsiyr-ul-Qur-aan al-´Adhwiym (1/311). Linganisha na Fath-ul-Baariy (8/199).
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fath Rabb-il-Bariyyah, uk. 45
- Imechapishwa: 14/01/2020
´Arshi kilugha ni kiti cha mfalme. Allaah (Ta´ala) amesema kuhusu Yuusuf:
وَرَفَعَ أَبَوَيْهِ عَلَى الْعَرْشِ
“Aliwainua wazazi wake wawili juu ya kiti cha ufalme.”[1]
Vilevile Amesema kuhusu malkia wa Saba´:
وَلَهَا عَرْشٌ عَظِيمٌ
“Na anacho kiti cha ufalme kikubwa.”[2]
Kuhusiana na ´Arshi ya Mwingi wa Rahmah ambayo amelingana juu yake, ni ´Arshi kubwa yenye kuwazunguka viumbe. ´Arshi ndio kiumbe kikubwa kabisa. Abu Dharr (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mbingu saba na ardhi saba ukizilinganisha na Kursiy ni kama mfano wa pete iliyotupwa kwenye jangwa. Na tofauti kati ya ´Arshi na Kursiy ni kama tofauti kati ya jangwa na pete hiyo.”[3]
Mtunzi wa kitabu Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah (Rahimahu Allaah) amesema katika “ar-Risaalah al-´Arshiyyah”:
“Hadiyth hii ina njia nyingi. Imepokelewa na Abu Haatim, Ibn Hibbaan katika “as-Swahiyh”, Ahmad katika “al-Musnad” na wengineo.
Maana ya al-Kursiy kilugha ni kiti ambacho mtu hukaa juu yake. Ama Kursiy ambayo Allaah amejinasibishia nayo ni mahali pa kuwekea miguu Yake miwili (Ta´ala). Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa) amesema:
“Kursiy ni mahala pa kuwekea miguu miwili na ´Arshi hakuna awezaye kuikadiria isipokuwa Allaah (´Azza wa Jall).”[4]
Maana hii iliyotajwa na Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa) ndio yenye kutangaa kwa Ahl-us-Sunnah. Hii ndio sahihi kutoka kwake tofauti na mapokezi yaliyopokelewa yenye kusema kuwa Kursiy maana yake ni elimu. Kadhalika tafsiri ya al-Hasan al-Baswriy yenye kusema kuwa Kursiy maana yake ni ´Arshi ni dhaifu kwa mujibu wa Ibn Kathiyr (Rahimahu Allaah)[5].
[1] 12:100
[2] 27:23
[3] Ibn Hibbaan (94 – al-Mawaarid), Abu Nu´aym katika ”al-Hilyah” (1/167) na al-´Adhwamah (2/569, 649).
[4] al-Haakim amesema:
”Ni Swahiyh juu ya sharti za al-Bukhaariy na Muslim.” (al-Mustadrak (2/282))
adh-Dhahabiy amesema:
”Wapokezi wake ni waaminifu.” (al-´Uluww, uk. 61)
al-Azhariy amesema:
“Wanachuoni wameafikiana juu ya usahihi wa upokezi huu.” (Tahdhib-ul-Lughah (10/61))
[5] Tafsiyr-ul-Qur-aan al-´Adhwiym (1/311). Linganisha na Fath-ul-Baariy (8/199).
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fath Rabb-il-Bariyyah, uk. 45
Imechapishwa: 14/01/2020
https://firqatunnajia.com/12-arshi/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)