Swali 12: Akitwahirika mwenye hedhi au mwenye damu ya uzazi wakati wa ´Aswr analazimika kulipa Dhuhr pamoja na ´Aswr au inayomlazimu ni ´Aswr peke yake?
Jibu: Maoni yenye nguvu katika masuala haya ni kwamba analazimika kulipa ´Aswr peke yake. Kwa sababu hakuna dalili juu ya ulazima wa kulipa Dhuhr. Msingi ni kutakasika kwa dhimmah. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Yule mwenye kuwahi Rak´ah moja ya swalah ya asubuhi kabla ya jua kuchomoza basi ameiwahi ´Aswr.”
Hakutaja kwamba ameiwahi Dhuhr. Dhuhr ingelikuwa ni lazima basi Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) angebainisha.
Jingine ni kwmaba mwanamke akipata hedhi baada ya kuingia wakati wa Dhuhr hakuna kinachomlazimu isipokuwa kulipa swalah ya Dhuhr pasi na swalah ya ´Aswr ingawa wakati fulani Dhuhr inakusanywa pamoja na ´Aswr. Hapana tofauti kati yake na sura ya swali lililoulizwa.
Kujengea juu ya haya ni kwamba maoni yenye nguvu ni kwamba hakuna kinachomlazimu isipokuwa kulipa ´Aswr peke yake kwa dalili ya andiko na kipimo.
Vivyo hivyo ndio hali endapo mwanamke atasafika kabla ya kumalizika kwa wakati wa ´Ishaa. Katika hali hiyo hakuna kinachomlazimu isipokuwa swalah ya ´Ishaa peke yake. Swalah ya Maghrib haimlazimu.
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: 60 su-aal wa jawaab fiy Ahkaam-il-Haydhw, uk. 13-14
- Imechapishwa: 20/06/2021
Swali 12: Akitwahirika mwenye hedhi au mwenye damu ya uzazi wakati wa ´Aswr analazimika kulipa Dhuhr pamoja na ´Aswr au inayomlazimu ni ´Aswr peke yake?
Jibu: Maoni yenye nguvu katika masuala haya ni kwamba analazimika kulipa ´Aswr peke yake. Kwa sababu hakuna dalili juu ya ulazima wa kulipa Dhuhr. Msingi ni kutakasika kwa dhimmah. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Yule mwenye kuwahi Rak´ah moja ya swalah ya asubuhi kabla ya jua kuchomoza basi ameiwahi ´Aswr.”
Hakutaja kwamba ameiwahi Dhuhr. Dhuhr ingelikuwa ni lazima basi Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) angebainisha.
Jingine ni kwmaba mwanamke akipata hedhi baada ya kuingia wakati wa Dhuhr hakuna kinachomlazimu isipokuwa kulipa swalah ya Dhuhr pasi na swalah ya ´Aswr ingawa wakati fulani Dhuhr inakusanywa pamoja na ´Aswr. Hapana tofauti kati yake na sura ya swali lililoulizwa.
Kujengea juu ya haya ni kwamba maoni yenye nguvu ni kwamba hakuna kinachomlazimu isipokuwa kulipa ´Aswr peke yake kwa dalili ya andiko na kipimo.
Vivyo hivyo ndio hali endapo mwanamke atasafika kabla ya kumalizika kwa wakati wa ´Ishaa. Katika hali hiyo hakuna kinachomlazimu isipokuwa swalah ya ´Ishaa peke yake. Swalah ya Maghrib haimlazimu.
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: 60 su-aal wa jawaab fiy Ahkaam-il-Haydhw, uk. 13-14
Imechapishwa: 20/06/2021
https://firqatunnajia.com/12-alipe-dhuhr-na-aswr-pamoja-na-maghrib-na-ishaa/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)