Swali: Mimi ni kijana ambaye yamenipata maradhi ya neva na nimefikwa na siku ambazo nashindwa kutamka al-Faatihah. Kuna ndugu nimemtuma kwa mmoja katika Mashaykh akanijibu kwamba inafaa kwangu kuswali kwa kiwango cha Rak´ah pasi na kisomo. Ni ipi hukumu ya hilo?
Jibu: Mola wetu amesema:
فَاتَّقُوا اللَّـهَ مَا اسْتَطَعْتُمْ
”Mcheni Allaah muwezavyo.” (64:16)
Muislamu akipatwa na jambo linalomfanya kushindwa kusoma, swalah yake inasihi. Atasimama kwa kiwango cha kusoma al-Faatihah na kilicho zaidi yake kidogo na kunamtosha. Akiweza kusema Subhaan Allaah, Alhamdulillaah, Laa ilaaha illa Allaah na Allaahu Akbar, basi itamuwajibikia kufanya hivo. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimwamrisha kufanya Tasbiyh, Tahmiyd, Tahliyl, Takbiyr na Laa hawlah wa quwattah illa bi Allaah yule ambaye alimlalamikia kushindwa kusoma al-Faatihah. Pia anaweza kusema yale yatayomkuwia wepesi katika mfano wa hayo. Anayeweza kufanya hivo basi atafanya mpaka pale atakapoweza kusoma al-Faatihah. Tunacholenga ni kwamba:
فَاتَّقُوا اللَّـهَ مَا اسْتَطَعْتُمْ
”Mcheni Allaah muwezavyo.”
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/4317/ما-حكم-صلاة-العاجز-عن-القراءة
- Imechapishwa: 06/06/2022
Swali: Mimi ni kijana ambaye yamenipata maradhi ya neva na nimefikwa na siku ambazo nashindwa kutamka al-Faatihah. Kuna ndugu nimemtuma kwa mmoja katika Mashaykh akanijibu kwamba inafaa kwangu kuswali kwa kiwango cha Rak´ah pasi na kisomo. Ni ipi hukumu ya hilo?
Jibu: Mola wetu amesema:
فَاتَّقُوا اللَّـهَ مَا اسْتَطَعْتُمْ
”Mcheni Allaah muwezavyo.” (64:16)
Muislamu akipatwa na jambo linalomfanya kushindwa kusoma, swalah yake inasihi. Atasimama kwa kiwango cha kusoma al-Faatihah na kilicho zaidi yake kidogo na kunamtosha. Akiweza kusema Subhaan Allaah, Alhamdulillaah, Laa ilaaha illa Allaah na Allaahu Akbar, basi itamuwajibikia kufanya hivo. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimwamrisha kufanya Tasbiyh, Tahmiyd, Tahliyl, Takbiyr na Laa hawlah wa quwattah illa bi Allaah yule ambaye alimlalamikia kushindwa kusoma al-Faatihah. Pia anaweza kusema yale yatayomkuwia wepesi katika mfano wa hayo. Anayeweza kufanya hivo basi atafanya mpaka pale atakapoweza kusoma al-Faatihah. Tunacholenga ni kwamba:
فَاتَّقُوا اللَّـهَ مَا اسْتَطَعْتُمْ
”Mcheni Allaah muwezavyo.”
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/4317/ما-حكم-صلاة-العاجز-عن-القراءة
Imechapishwa: 06/06/2022
https://firqatunnajia.com/111491-2/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)