11. Hadiyth “Nilikuwa pamoja na Ibn ´Umar ´Arafaat… “

48- Anas bin Siyriyn amesema:

“Nilikuwa pamoja na Ibn ´Umar (Rahimahu Allaah) ´Arafaat. Alipoondoka nikaondoka pamoja naye. Mpaka alipokuja imamu akaswali naye swalah ya kwanza na ´Aswr. Kisha akasimama pamoja nami na marafiki zangu mpaka imamu alipoondoka nasi tukawa tumeondoka naye. Mpaka alipofika sehemu ya kupita mlima akampigisha mnyama wake magoti nasi tukafanya vivyo hivyo. Tulifikiri kuwa anataka kuswali. Mtumwa wake ambaye anamshikia mnyama wake akasema: “Hafikirii kuswali. Lakini amekumbuka kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipofika sehemu hii alikidhi haja yake ambapo na yeye akapenda akidhi haja yake.”

Ameipokea Ahmad na wapokezi wake ni wenye kujengewa hoja katika upokezi wa kwanza wa al-Bukhaariy.

Kuna mapokezi mengi mno kutoka kwa Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhumaa) juu ya kumfuata kwake na kutendea kazi Sunnah zake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Adhwiym bin ´Abdil-Qawiy al-Mundhiriy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/127)
  • Imechapishwa: 26/04/2020
  • taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy