734- Haarithah bin an-Nu´maan (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Mmoja wenu anachukua mifugo yake na akashuhudia swalah katika mkusanyiko. Wakati ulivokuwa unaenda chakula cha mifugo yake kikaisha anasema: “Ningewatafutia mifugo yangu sehemu ambayo ina malisho mengi zaidi kuliko hapa.” Hivyo anahama na wala hashuhudii isipokuwa swalah ya ijumaa moja. . Wakati ulivokuwa unaenda chakula cha mifugo yake kikaisha anasema: “Ningewatafutia mifugo yangu sehemu ambayo ina malisho mengi zaidi kuliko hapa.” Hivyo anahama na wala hashuhudii swalah ya ijumaa wala swalah ya mkusanyiko. Matokeo yake Allaah anampiga muhuri katika moyo wake.”[1]

Ameipokea Ahmad kupitia kwa ´Umar bin ´Abdillaah, mtumwa aliyeachwa huru na Ghufrah. Ni mwaminifu kwa mtazamo wake[2].

[1] Nzuri kupitia zengine.

[2] Ni mnyonge kwa mtazamo wa wanachuoni wengi na ndio maana al-Haythamiy na al-´Asqalaaniy wakamdhoofisha. Hata hivyo inatiliwa nguvu na Hadiyth ya kabla yake.

  • Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/453)
  • Imechapishwa: 26/04/2020
  • taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy