Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
Kauli Yake (Ta´ala):
وَمَا تَكُونُ فِي شَأْنٍ وَمَا تَتْلُو مِنْهُ مِن قُرْآنٍ وَلَا تَعْمَلُونَ مِنْ عَمَلٍ إِلَّا كُنَّا عَلَيْكُمْ شُهُودًا إِذْ تُفِيضُونَ فِيهِ
“Hushughuliki katika jambo lolote wala husomi humo chochote katika Qur-aan na wala hamtendi ‘amali yoyote isipokuwa Tunakuwa ni mashahidi juu yenu mnaposhughulika nayo.”[1]
MAELEZO
Hii ni dalili ya ngazi ya pili:
وَمَا تَكُونُ فِي شَأْنٍ
“Hushughuliki katika jambo lolote… “
Hapa anazungumzishwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika jambo lolote unalokuwemo. Ni mamoja katika mambo ya ´ibaadah au mengineyo katika matendo yote, kutikisika kwako na mengineyo.
وَمَا تَتْلُو مِنْهُ مِن قُرْآنٍ
“… wala husomi humo chochote katika Qur-aan… “
Bi maana kutoka kwa Allaah kwa sababu Qur-aan ni yenye kutoka kwa Allaah (´Azza wa Jall). Vilevile kuna uwezekano dhamira ikawa ni yenye kurudi katika shani. Hivyo itakuwa na maana kwamba katika hali ambayo unakuwa ni mwenye kusoma Qur-aan.
وَلَا تَعْمَلُونَ مِنْ عَمَلٍ
“… wala hamtendi ‘amali yoyote… “
Hapa ni kwa Ummah mzima; kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na wengineo. Inahusiana na matendo ya kheri na matendo ya shari.
إِلَّا كُنَّا عَلَيْكُمْ شُهُودً
“… isipokuwa Tunakuwa ni mashahidi… “
Bi maana tunakuona na tunakushuhudieni. Hii ni dalili ya maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“… basi Yeye anakuona.”
إِذْ تُفِيضُونَ فِيهِ
“… mnaposhughulika nayo.”
Mnapoibashiri na kuifanya. Hapa kuna dalili juu ya ngazi ya pili katika ngazi za Ihsaan na kwamba Yeye (Jalla wa ´Alaa) anamuona kila mtendaji kwa kitendo chake. Anamuona (Subhaanahu wa Ta´ala) na anamjua. Hafichiki Kwake:
إِنَّ اللَّـهَ لَا يَخْفَىٰ عَلَيْهِ شَيْءٌ فِي الْأَرْضِ وَلَا فِي السَّمَاءِ
“Hakika Allaah hakifichiki Kwake chochote katika ardhi wala katika mbingu.”[2]
[1] 10:61
[2] 03:05
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Thalaathat-il-Usuwl, uk. 226-227
- Imechapishwa: 27/01/2021
Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
Kauli Yake (Ta´ala):
وَمَا تَكُونُ فِي شَأْنٍ وَمَا تَتْلُو مِنْهُ مِن قُرْآنٍ وَلَا تَعْمَلُونَ مِنْ عَمَلٍ إِلَّا كُنَّا عَلَيْكُمْ شُهُودًا إِذْ تُفِيضُونَ فِيهِ
“Hushughuliki katika jambo lolote wala husomi humo chochote katika Qur-aan na wala hamtendi ‘amali yoyote isipokuwa Tunakuwa ni mashahidi juu yenu mnaposhughulika nayo.”[1]
MAELEZO
Hii ni dalili ya ngazi ya pili:
وَمَا تَكُونُ فِي شَأْنٍ
“Hushughuliki katika jambo lolote… “
Hapa anazungumzishwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika jambo lolote unalokuwemo. Ni mamoja katika mambo ya ´ibaadah au mengineyo katika matendo yote, kutikisika kwako na mengineyo.
وَمَا تَتْلُو مِنْهُ مِن قُرْآنٍ
“… wala husomi humo chochote katika Qur-aan… “
Bi maana kutoka kwa Allaah kwa sababu Qur-aan ni yenye kutoka kwa Allaah (´Azza wa Jall). Vilevile kuna uwezekano dhamira ikawa ni yenye kurudi katika shani. Hivyo itakuwa na maana kwamba katika hali ambayo unakuwa ni mwenye kusoma Qur-aan.
وَلَا تَعْمَلُونَ مِنْ عَمَلٍ
“… wala hamtendi ‘amali yoyote… “
Hapa ni kwa Ummah mzima; kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na wengineo. Inahusiana na matendo ya kheri na matendo ya shari.
إِلَّا كُنَّا عَلَيْكُمْ شُهُودً
“… isipokuwa Tunakuwa ni mashahidi… “
Bi maana tunakuona na tunakushuhudieni. Hii ni dalili ya maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“… basi Yeye anakuona.”
إِذْ تُفِيضُونَ فِيهِ
“… mnaposhughulika nayo.”
Mnapoibashiri na kuifanya. Hapa kuna dalili juu ya ngazi ya pili katika ngazi za Ihsaan na kwamba Yeye (Jalla wa ´Alaa) anamuona kila mtendaji kwa kitendo chake. Anamuona (Subhaanahu wa Ta´ala) na anamjua. Hafichiki Kwake:
إِنَّ اللَّـهَ لَا يَخْفَىٰ عَلَيْهِ شَيْءٌ فِي الْأَرْضِ وَلَا فِي السَّمَاءِ
“Hakika Allaah hakifichiki Kwake chochote katika ardhi wala katika mbingu.”[2]
[1] 10:61
[2] 03:05
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Thalaathat-il-Usuwl, uk. 226-227
Imechapishwa: 27/01/2021
https://firqatunnajia.com/108-dalili-ya-ihsaan-katika-qur-aan-ii/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)