Ilipokuwa imewekwa katika Shari´ah kusimama na kujitahidi usiku wenye cheo na nyusiku za Ramadhaan ndipo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akazindua jambo hilo na akahimiza Ummah kusimama na yeye mweneywe akafanya hivo. al-Bukhaariy na Muslim wamepokea kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliyesema:
“Yeyote atakayesimama usiku wenye cheo kwa imani na kwa matarajio, basi Allaah atamsamehe madhambi yake yaliyotangulia.”
Endapo usiku wa nusu ya Sha´baan, usiku wa ijumaa ya kwanza ya Rajab, usiku wa Israa´ na Mi´raaj imesuniwa kuufanya maalum kwa sherehe au chochote katika ´ibaadah basi Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) angewaelekeza Ummah katika jambo hilo au yeye mwenyewe angefanya hivo. Iwapo angefanya chochote katika hayo basi Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) wangewanukulia Ummah na wasingewaficha. Kwani wao ndio watu bora na wenye kuwatakia mema zaidi watu baada ya Mitume (Swalla Allaahu ´alayhim wa sallam) na Allaah awawie radhi Maswahabah wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) nao wamemridhia.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: at-Tahdhiyr minal-Bid´ah, uk. 31-32
- Imechapishwa: 19/01/2022
Ilipokuwa imewekwa katika Shari´ah kusimama na kujitahidi usiku wenye cheo na nyusiku za Ramadhaan ndipo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akazindua jambo hilo na akahimiza Ummah kusimama na yeye mweneywe akafanya hivo. al-Bukhaariy na Muslim wamepokea kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliyesema:
“Yeyote atakayesimama usiku wenye cheo kwa imani na kwa matarajio, basi Allaah atamsamehe madhambi yake yaliyotangulia.”
Endapo usiku wa nusu ya Sha´baan, usiku wa ijumaa ya kwanza ya Rajab, usiku wa Israa´ na Mi´raaj imesuniwa kuufanya maalum kwa sherehe au chochote katika ´ibaadah basi Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) angewaelekeza Ummah katika jambo hilo au yeye mwenyewe angefanya hivo. Iwapo angefanya chochote katika hayo basi Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) wangewanukulia Ummah na wasingewaficha. Kwani wao ndio watu bora na wenye kuwatakia mema zaidi watu baada ya Mitume (Swalla Allaahu ´alayhim wa sallam) na Allaah awawie radhi Maswahabah wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) nao wamemridhia.
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: at-Tahdhiyr minal-Bid´ah, uk. 31-32
Imechapishwa: 19/01/2022
https://firqatunnajia.com/10-yangethibiti-basi-tungenakiliwa/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)