10. Dalili ya nane kutoka katika Sunnah kwamba Allaah yuko juu ya viumbe

8- Muhammad bin ´Abdil-Baaqiy alisomewa na mimi huku nasikiliza: Ahmad bin ´Aliy bin al-Husayn amekukhabarisheni: Hibatullaah bin al-Hasan ametuhadithia: ´Ubaydullaah bin Ahmad bin ´Aliy ametuhadithia: ´Abdullaah bin Muhammad bin Ziyaad ametuhadithia: Muhammad bin Ghaalib al-Antwaakiy ametuhadithia: Yahyaa bin as-Sakan ametuhadithia, kutoka kwa Shu´bah na Qays, kutoka kwa Ishaaq, kutoka kwa Abu ´Ubaydah, kutoka kwa baba yake aliyesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Wahurumieni wale walioko ardhini atakuhurumieni Yule aliye juu ya mbingu.”[1]

[1] al-Laalakaa’iy katika ”Sharh Usuul I´tiqaad Ahl-is-Sunnah wal-Jamaa´ah” (655), ad-Daarimiy katika ”ar-Radd ´alaal-Jahmiyyah”, uk. 20, na al-Haakim aliyesema:

”Mlolongo wa wapokezi ni Swahiyh.” (al-Mustadrak (4/248))

  • Mhusika: Imaam Muwaffaq-ud-Diyn bin Qudaamah al-Maqdisiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Ithbaatu Swifat-il-´Uluww, uk. 79-80
  • Imechapishwa: 16/04/2018