09. Allaah aliumba Pepo na Moto kabla ya kuumba viumbe

[16] Kuamini kwamba Allaah aliumba Pepo na Moto kabla ya kuumba viumbe. Neema za Peponi zitaendelea kuwepo milele na kamwe wanawake wa Peponi hawakutokufa.

Adhabu ya Motoni ni yenye kudumu na watu wake ambao walitengana na dunia hii hali ya kuwa si wenye kumwabudu Allaah pekee na si wenye kufuata Sunnah, watadumishwa humo.

[17] Kuhusiana na wapwekeshaji watenda madhambi, watatolewa humo ndani kwa uombezi. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

”Uombezi wangu ni kwa ajili ya watenda madhambi makubwa kutoka katika Ummah wangu.”[1]

Watoto wa washirikina watakuwa Motoni.

[1] Ahmad (3/213), Abu Daawuud (4739) na at-Tirmidhiy (2345).

  • Mhusika: Imaam Abul-Husayn Muhammad bin Abiy Ya´laa al-Hanbaliy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Kitaab-ul-I´tiqaad, uk. 34
  • Imechapishwa: 25/02/2019