Hizi ndio sampuli tatu za Tawhiyd:
1- Tawhiyd-ur-Rubuubiyyah. Aina hii mara nyingi hakuna yeyote mwenye kuipinga.
2- Tawhiyd-ul-Uluuhiyyah. Aina hii wengi wanaipinga na hakuna wenye kuithibitisha isipokuwa tu wafuasi wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Amesema (Ta´ala):
وَإِن تُطِعْ أَكْثَرَ مَن فِي الْأَرْضِ يُضِلُّوكَ عَن سَبِيلِ اللَّـهِ
“Ukiwatii wengi walioko ulimwenguni, basi watakupoteza kutokamana na njia ya Allaah.”[1]
وَمَا يُؤْمِنُ أَكْثَرُهُم بِاللَّـهِ إِلَّا وَهُم مُّشْرِكُونَ
”Wengi kati yao hawamwamini Allaah isipokuwa wao ni wenye kufanya shirki.”[2]
Hakuna walioithibitisha Tawhiyd-ul-Uluuhiyyah isipokuwa tu wafuasi wa Mitume. Ni waumini wa kila nyumati. Wameithibitisha Tawhiyd-ul-Uluuhiyyah na washirikina wa kila zama na mahali wakaipinga.
3- Tawhiyd-ul-Asmaa´ was-Swifaat. Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah wanathibitisha majina na sifa za Allaah. Sambamba na hilo Jahmiyyah, Mu´tazilah, Ashaa´irah na vifaranga vyao wanaikengeusha na kuzipindisha maana. Baadhi yao wamezikanusha zote kwa ujumla na wengine baadhi yake. Muhimu ni kujua namna wanavyoamini Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah katika jambo hili.
[1] 06:116
[2] 12:106
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: I´aanat-ul-Mustafiyd bi Sharh Kitaab-it-Tawhiyd, uk. 25
- Imechapishwa: 23/07/2019
Hizi ndio sampuli tatu za Tawhiyd:
1- Tawhiyd-ur-Rubuubiyyah. Aina hii mara nyingi hakuna yeyote mwenye kuipinga.
2- Tawhiyd-ul-Uluuhiyyah. Aina hii wengi wanaipinga na hakuna wenye kuithibitisha isipokuwa tu wafuasi wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Amesema (Ta´ala):
وَإِن تُطِعْ أَكْثَرَ مَن فِي الْأَرْضِ يُضِلُّوكَ عَن سَبِيلِ اللَّـهِ
“Ukiwatii wengi walioko ulimwenguni, basi watakupoteza kutokamana na njia ya Allaah.”[1]
وَمَا يُؤْمِنُ أَكْثَرُهُم بِاللَّـهِ إِلَّا وَهُم مُّشْرِكُونَ
”Wengi kati yao hawamwamini Allaah isipokuwa wao ni wenye kufanya shirki.”[2]
Hakuna walioithibitisha Tawhiyd-ul-Uluuhiyyah isipokuwa tu wafuasi wa Mitume. Ni waumini wa kila nyumati. Wameithibitisha Tawhiyd-ul-Uluuhiyyah na washirikina wa kila zama na mahali wakaipinga.
3- Tawhiyd-ul-Asmaa´ was-Swifaat. Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah wanathibitisha majina na sifa za Allaah. Sambamba na hilo Jahmiyyah, Mu´tazilah, Ashaa´irah na vifaranga vyao wanaikengeusha na kuzipindisha maana. Baadhi yao wamezikanusha zote kwa ujumla na wengine baadhi yake. Muhimu ni kujua namna wanavyoamini Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah katika jambo hili.
[1] 06:116
[2] 12:106
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: I´aanat-ul-Mustafiyd bi Sharh Kitaab-it-Tawhiyd, uk. 25
Imechapishwa: 23/07/2019
https://firqatunnajia.com/09-aina-tatu-za-tawhiyd/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)