182 – ´Uthmaan (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Ambaye atatawadha na akaeneza vizuri wudhuu´ wake, basi huondoka madhambi yake kutoka mwilini mwake mpaka yakaondoka kutoka chini ya kucha zake.”[1]
Katika upokezi mwingine imekuja:
“´Uthmaan alitawadha kisha akasema: “Nilimwona Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akitawadha mfano wa wudhuu´ wangu huu. Kisha akasema: “Yule ambaye atatawadha namna hii, basi atasamehewa yale madhambi yake yaliyotangulia na swalah yake na kutembea kwake kwenda msikitini itakuwa ni ziada ya thawabu.”
Ameipokea Muslim na an-Nasaa´iy kwa ufupi ambapo tamko lake ni kama ifuatavyo:
“Hakuna mtu yeyote atakayetawadha ambapo akafanya vizuri wudhuu´ wake isipokuwa atasamehewa [madhambi] yaliyoko kati yake na swalah nyingine atakayoiswali.”
Cheni ya wapokezi wake iko kwa mujibu wa sharti za al-Bukhaariy na Muslim. Ibn Khuzaymah pia ameipokea katika “as-Swahiyh” yake kwa ufupi kama ulivyo upokezi wa an-Nasaa´iy. Aidha Ibn Maajah ameipokea kwa ufupi na ameongeza mwishoni mwake kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Hata hivyo asighurike yeyote.”[2]
Katika tamko la an-Nasaa´iy imekuja:
“Yule atakayekamilisha wudhuu´ kama alivyoamrisha Allaah (Ta´ala), basi zile swalah tano zitakuwa ni kifutio cha madhambi kwa yale yaliyoko baina yazo.”
[1] Swahiyh.
[2] Cheni ya wapokezi ni Swahiyh kwa mujibu wa sharti za al-Bukhaariy na Muslim, hata hivyo imekuja kwa tamko linalosema:
”Yule ambaye atatawadha namna hii, halafu akasimama na kuswali Rak´ah mbili, basi atasamehewa yale madhambi yake yaliyotangulia.” Kisha akasema: “Hata hivyo msighurike.”
al-Bukhaariy ameipokea kwa tamko hili.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Adhwiym bin ´Abdil-Qawiy al-Mundhiriy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/189-190)
- Imechapishwa: 14/04/2021
- taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
182 – ´Uthmaan (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Ambaye atatawadha na akaeneza vizuri wudhuu´ wake, basi huondoka madhambi yake kutoka mwilini mwake mpaka yakaondoka kutoka chini ya kucha zake.”[1]
Katika upokezi mwingine imekuja:
“´Uthmaan alitawadha kisha akasema: “Nilimwona Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akitawadha mfano wa wudhuu´ wangu huu. Kisha akasema: “Yule ambaye atatawadha namna hii, basi atasamehewa yale madhambi yake yaliyotangulia na swalah yake na kutembea kwake kwenda msikitini itakuwa ni ziada ya thawabu.”
Ameipokea Muslim na an-Nasaa´iy kwa ufupi ambapo tamko lake ni kama ifuatavyo:
“Hakuna mtu yeyote atakayetawadha ambapo akafanya vizuri wudhuu´ wake isipokuwa atasamehewa [madhambi] yaliyoko kati yake na swalah nyingine atakayoiswali.”
Cheni ya wapokezi wake iko kwa mujibu wa sharti za al-Bukhaariy na Muslim. Ibn Khuzaymah pia ameipokea katika “as-Swahiyh” yake kwa ufupi kama ulivyo upokezi wa an-Nasaa´iy. Aidha Ibn Maajah ameipokea kwa ufupi na ameongeza mwishoni mwake kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Hata hivyo asighurike yeyote.”[2]
Katika tamko la an-Nasaa´iy imekuja:
“Yule atakayekamilisha wudhuu´ kama alivyoamrisha Allaah (Ta´ala), basi zile swalah tano zitakuwa ni kifutio cha madhambi kwa yale yaliyoko baina yazo.”
[1] Swahiyh.
[2] Cheni ya wapokezi ni Swahiyh kwa mujibu wa sharti za al-Bukhaariy na Muslim, hata hivyo imekuja kwa tamko linalosema:
”Yule ambaye atatawadha namna hii, halafu akasimama na kuswali Rak´ah mbili, basi atasamehewa yale madhambi yake yaliyotangulia.” Kisha akasema: “Hata hivyo msighurike.”
al-Bukhaariy ameipokea kwa tamko hili.
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Adhwiym bin ´Abdil-Qawiy al-Mundhiriy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/189-190)
Imechapishwa: 14/04/2021
taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
https://firqatunnajia.com/07-hadiyth-ambaye-atatawadha-na-akaeneza-vizuri-wudhuu-wake/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)